Mezali 29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona. 2 Wenye haki wakiongozeka, watu wanafurahi. Lakini waovu wakitawala, watu wanalalamika. 3 Anayependa hekima anamufurahisha baba yake; lakini anayeandamana na kahaba anapoteza mali yake. 4 Mufalme akifuata sheria ya Mungu, anaimarisha inchi. Lakini akipenda kituliro, taifa linaangamia. 5 Mwenye kumubembeleza jirani yake, anatega mutego wa kujinasa mwenyewe. 6 Mutu mubaya ananaswa kwa kosa lake, lakini mutu wa haki anaimba na kufurahi. 7 Mwenye haki anajua haki za wamasikini, lakini mutu mwovu hajui mambo hayo. 8 Wenye mazarau wanaleta mavurugo katika muji muzima, lakini wenye hekima wanatuliza kasirani. 9 Mwenye hekima akibishana na mupumbafu, akasirike au acheke, ni mamoja; hatatulia. 10 Wanaopenda kumwanga damu wanachukia mutu mukamilifu, lakini watu wa usawa wanalinda maisha yake. 11 Mupumbafu anaonyesha hasira yake wazi, lakini mwenye hekima anaizuia na kuituliza. 12 Mutawala akisikiliza mambo ya uongo, wakubwa wake wote watakuwa waovu. 13 Masikini na mugandamizaji wanafanana kwa kitu kimoja: wote wawili wamepewa macho na Yawe. 14 Mufalme anayewaamua wamasikini kwa haki, ataona utawala wake unaimarika milele. 15 Azabu na maonyo vinaleta hekima, lakini mutoto aliyeachiliwa anapatisha mama yake haya. 16 Waovu wakiongozeka, zambi zinaongezeka. Lakini wenye haki watashuhudia kuanguka kwao. 17 Umwazibu mwana wako naye hatakupa wasiwasi; yeye atafurahisha moyo wako. 18 Pasipo maono ya kinabii, watu wanashindwa kujizuiza. Heri mutu yule anayeshika sheria. 19 Mutumwa haonyeki kwa maneno matupu; maana ingawa anayaelewa, yeye hatayatii. 20 Unamwona mutu anayesema bila kufikiri? Mutu mupumbafu ni afazali kuliko yeye. 21 Anayebembeleza mutumwa wake tangu utoto, kwa mwisho mutumwa yule atamurizi. 22 Mwenye kasirani anachochea ugomvi, mutu wa hasira anasababisha makosa mengi. 23 Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima. 24 Anayeshirikiana na mwizi anajizuru mwenyewe; anasikia laana ikitolewa bila kusema neno. 25 Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama. 26 Wengi wanapenda kujipendekeza kwa mutawala, lakini mutu anapata haki yake kwa Yawe. 27 Mwovu ni chukizo kwa mwenye haki, naye mwenye haki ni chukizo kwa mwovu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo