Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mezali 27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Usijisifie kwa ajili ya kesho. Haujui siku ya leo itakuletea nini.

2 Acha watu wengine wakusifu, kuliko kujisifu kwa mudomo wako wewe mwenyewe.

3 Jiwe ni zito na muchanga vilevile, lakini uchokozi wa mupumbafu ni muzito zaidi.

4 Kasirani ni kali na hasira inaangamiza; lakini ni nani anayeweza kupingana na wivu?

5 Afazali mutu anayekuonya waziwazi, kuliko yule anayeficha upendo.

6 Makaripio ya rafiki yanaonyesha uaminifu, lakini busu la adui ni udanganyifu.

7 Aliyeshiba anakataa hata asali, lakini kwa mwenye njaa kila chakula kichungu ni kitamu.

8 Mutu aliyepotea mbali na kwake ni kama ndege aliyepotea mbali na chicha yake.

9 Mafuta na marasi vinafurahisha moyo, vilevile utamu wa urafiki kuliko kujitoshelea mwenyewe.

10 Usisahau warafiki zako wala wa baba yako. Ukipatwa na magumu usikimbilie kwa ndugu yako. Afazali jirani ambaye iko karibu kuliko ndugu anayekuwa mbali.

11 Ukuwe na hekima, mwana wangu, upate kunifurahisha moyo, nami sitakosa neno la kumujibu mutu yeyote anayenizarau.

12 Mwenye akili anaona hatari na kujificha, lakini wajinga wanajitokeza mbele na kuumia.

13 Mutu akiahidi mbele yako kubeba muzigo wa mutu mwingine, unyanganye nguo yake; utwae rehani kwake maana amebeba muzigo wa mutu mwingine.

14 Anayemusalimia jirani yake kwa kelele asubui mapema, itahesabiwa kwamba amemutakia laana.

15 Muke mugomvi ni kama matone ya mvua yasiyoisha siku ya mvua.

16 Kumuzuia ni sawa na kuzuia upepo, au kukamata mafuta kwa mukono.

17 Chuma kinanoa chuma, vilevile mutu anafundishwa na mwenzake.

18 Anayetunza muti wa tini atakula matunda yake. Anayetumikia bwana wake ataheshimiwa.

19 Kama uso unavyojiona wenyewe katika maji, ndivyo mutu anavyojijua mwenyewe ndani ya moyo.

20 Kuzimu na shimo la kuangamia havishibi hata kidogo, vilevile macho ya watu hayashibi.

21 Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, na mutu anapimwa kutokana na sifa zake.

22 Hata kama ukitwanga mupumbafu katika kinu, sawa na ngano, hautaweza kumutenganisha na upumbafu wake.

23 Angalia vizuri hali ya makundi yako ya nyama; tunza vizuri nyama wako.

24 Maana utajiri haudumu milele, wala taji haidumu kwa vizazi vyote.

25 Nyuma ya kukata majani, wakati nyasi zinachipuka upya, kusanya majani toka kwenye milima.

26 Kondoo watakupatia sufu kwa ajili ya nguo zako, mbuzi nao utawauzisha na kujinunulia mashamba;

27 watakupa maziwa ya kukutoshelea na jamaa yako, na kwa ajili ya wajakazi wako.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan