Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mezali 21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Moyo wa mufalme ni kama maji yanayotiririka; Yawe anauongoza popote anapopenda.

2 Matendo yote ya mutu ni sawa katika macho yake, lakini Yawe anapima mioyo.

3 Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.

4 Macho ya kiburi na moyo wa majivuno vinaonyesha wazi zambi ya waovu.

5 Mipango ya mutu wa bidii inaleta mali kwa wingi, lakini kila mutu anayetenda kwa harakaharaka anapata umasikini.

6 Mali inayopatikana kwa udanganyifu ni muvuke unaopita na mutego wa kifo.

7 Ukali wa waovu utawaangamiza, maana wanakataa kutenda mambo ya haki.

8 Njia ya mutu mwenye kosa imepotoka, lakini mwenendo wa mwenye moyo safi ni sawa.

9 Afazali kuishi pembeni juu ya paa, kuliko kuishi ndani ya nyumba pamoja na mwanamuke mugomvi.

10 Mutu mwovu anatamani kutenda uovu; hata kwa jirani yake hana huruma.

11 Mwenye kiburi anapoazibiwa, mujinga anapata hekima. Ukimufundisha mwenye hekima, unamupatia maarifa.

12 Mwenye haki anajua yanayokuwa katika nyumba ya waovu: waovu wanaangushwa chini na kuangamia.

13 Anayekataa kusikia kilio cha masikini hatasikilizwa atakapolilia musaada.

14 Hasira inatulizwa kwa zawadi ya siri; kituliro kinachotolewa kwa uficho kinatuliza kasirani.

15 Haki ya sheria ikifuatwa, watu wema wanafurahi lakini watu waovu wanafazaika.

16 Anayetangatanga mbali na njia ya ufahamu, atajikuta ametua kati ya wafu.

17 Anayependa raha atakuwa masikini; anayefikiria tu kula na kunywa hatatajirika.

18 Mwovu atakuwa malipo kwa ukombozi wa wenye haki; nao wasiokuwa waaminifu kwa pahali pa watu wa usawa.

19 Afazali kuishi katika jangwa kuliko kukaa na mwanamuke mugomvi na muchokozi.

20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna hazina za bei kali, lakini mupumbafu anaponda mali yake yote.

21 Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.

22 Mwenye hekima anaweza kuteka muji wa wenye nguvu na kukiporomosha kikingio wanachokitegemea.

23 Anayechunga kinywa chake na ulimi wake, anajiepusha na matatizo.

24 Mwenye kiburi na majivuno jina lake ni “Mazarau”; anatenda kwa kujivuna tu.

25 Muvivu anakufa kwa kutokutimizwa kwa tamaa zake, maana mikono yake haitaki kufanya kazi.

26 Muchana kutwa mwovu anatamani kupata kitu, lakini mwenye haki anatoa, tena bila mipaka.

27 Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.

28 Mushuhuda mwongo ataangamia, lakini anayejua kusikiliza hawezi kunyamazishwa.

29 Mutu mwovu anajionyesha kuwa hodari, lakini mutu wa usawa anafikiri vizuri juu ya mwenendo wake.

30 Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.

31 Farasi anatayarishwa kwa vita, lakini ushindi unaletwa na Yawe.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan