Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mezali 20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Divai inaleta mazarau na kileo kinaleta ugomvi; yeyote anayevutwa navyo hana hekima.

2 Kasirani kali ya mufalme ni kama simba anayenguruma; anayemukasirikisha anahatarisha maisha yake.

3 Ni jambo la heshima kuepuka ugomvi; wapumbafu ndio wanaogombana.

4 Muvivu halimi wakati wa kulima; wakati wa mavuno atatafuta lakini hatapata kitu.

5 Mafikiri ya mutu ndani ya moyo wake ni kama kilindi cha maji; lakini mutu mwenye akili anajua kuyachota mule.

6 Watu wengi wanajivunia kuwa wema, lakini mwaminifu wa kweli anapatikana wapi?

7 Heri watoto wa mutu wa haki mwenye mwenendo mukamilifu!

8 Mufalme anapoikaa kwa kutoa hukumu, anapepeta uovu wote kwa macho yake.

9 Nani anayesubutu kusema: “Nimetakasa moyo wangu; mimi nimetakasika na zambi yangu?”

10 Mizani danganyifu na vipimo danganyifu, vyote ni chukizo kwa Yawe.

11 Hata mutoto anajulikana kwa matendo yake, kama ni safi na sawa.

12 Sikio linalosikia na jicho linaloona, vyote viwili vimefanywa na Yawe.

13 Usipende usingizi usikuje kuwa masikini; ukuwe macho nawe utakuwa na chakula kingi.

14 Mununuzi analalamika: “Hakifai, hakifai,” lakini akiondoka anajisifu amepunguziwa bei.

15 Kuna zahabu na wingi wa mawe ya bei kali; lakini kitu cha bei kali zaidi ni maneno ya maarifa!

16 Mutu akiahidi kumukopesha mutu asiyejulikana, unyanganye nguo yake kuwa rehani.

17 Chakula kinachopatikana kwa udanganyifu ni kitamu, lakini nyuma kinakuwa kama muchanga ndani ya kinywa.

18 Mipango mizuri inafanyika kwa kushauriana; ukitaka kuanza vita inafaa kufikiri kwanza.

19 Mupiga domo hafichi siri. Kwa hiyo umwepuke mutu wa kusemasema.

20 Anayemulaani baba yake au mama yake, mwangaza wa uzima wake utazimika kama taa katika giza.

21 Mali iliyopatikana kwa haraka kwa mwanzo, haitakuwa ya heri kwa mwisho.

22 Usiseme: “Nitalipiza ubaya niliotendewa.” Umutegemee Yawe naye atakusaidia.

23 Mizani danganyifu ni chukizo kwa Yawe, na vipimo visivyokuwa vya haki ni kitu kibaya.

24 Hatua za mutu zinaongozwa na Yawe; mwanadamu anaweza namna gani kuelewa njia yake?

25 Ni hatari kusema kwa muzaha “Nitamutolea Mungu hiki!” na kuanza kufikiri nyuma ya kufanya naziri ile.

26 Mufalme mwenye hekima anapepeta waovu; anawaazibu bila huruma.

27 Zamiri ya mutu ni taa ya Yawe; inachunguza nafsi ya mutu mpaka ndani kabisa.

28 Wema na uaminifu unamukinga mufalme; utawala wake unaimarishwa kwa haki.

29 Utukufu wa vijana ni nguvu zao. Uzuri wa wazee ni kichwa chenye imvi.

30 Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu; fimbo inasafisha nafsi mpaka ndani kabisa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan