Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mezali 19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Afazali masikini mwenye mwenendo mukamilifu kuliko mutu mupotovu wa maneno na mupumbafu.

2 Haifai mutu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka anajikwaa.

3 Mutu akijiangamiza kwa upumbafu wake, anaielekeza hasira yake kwa Yawe.

4 Mali inavuta warafiki wengi wapya, lakini masikini anaachwa na rafiki yake.

5 Mushuhuda mwongo hatakosa kuazibiwa; anayesema uongo hataepuka azabu.

6 Watu wengi wanajipendekeza kwa wakubwa; kila mutu anataka kuwa rafiki wa mutu mwenye kupana.

7 Masikini anachukiwa na wandugu zake; warafiki zake ndio zaidi: wanamukimbia! Hata awabembeleze namna gani, hatawapata.

8 Anayejipatia hekima anapenda nafsi yake; anayeshika ufahamu atastawi.

9 Mushuhuda mwongo hatakosa kuazibiwa; anayesema uongo ataangamia.

10 Haifai kwa mupumbafu kuishi kwa raha; tena ni vibaya zaidi mutumwa kuwatawala wakubwa.

11 Mwenye akili hakasiriki upesi; kusamehe makosa ni utukufu kwake.

12 Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.

13 Mutoto mupumbafu ni hasara kwa baba yake; na ugomvi wa muke ni kama matone ya mvua yasiyoisha.

14 Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.

15 Uvivu ni kama usingizi muzito; mutu muvivu atateseka kwa njaa.

16 Anayeshika amri analinda maisha yake; anayezarau agizo atakufa.

17 Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.

18 Azibu mwana wako wakati kungali bado tumaini lakini usitafute kumwangamiza.

19 Mutu wa hasira kali anapaswa kupata azabu; ukimwachilia mara moja itakuomba kumwachilia tena.

20 Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa kwa siku zinazokuja.

21 Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.

22 Kitu kinachotakiwa kwa mutu ni uaminifu; afazali mutu masikini kuliko mutu mwongo.

23 Kumwogopa Yawe kunaongoza kwenye uzima; anayemwogopa anajaliwa pumziko la kutoshelea, wala hatapatwa na ubaya wowote.

24 Muvivu anatia mukono wake katika sahani lakini hauinui mpaka kwenye midomo.

25 Umwazibu mwenye kuzarau naye mujinga atapata akili; umwonye mwenye akili naye atapata maarifa.

26 Anayemutesa baba yake na kumufukuza mama yake ni mutoto asiyefaa na mupotovu.

27 Mwana wangu, ukiacha kusikiliza mafundisho, mara moja utapotea mbali na maneno ya maarifa.

28 Mushuhuda asiyefaa kitu anazarau sheria ya Mungu; na kinywa cha mwovu kinameza uovu.

29 Azabu iko tayari kwa wenye kuzarau, na mapigo kwa migongo ya wapumbafu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan