Mezali 18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema. 2 Mupumbafu hapendezwi na ufahamu; kitu cha maana kwake ni maoni yake tu. 3 Mwovu anapokuja, mazarau yanakuja vilevile; pamoja na haya, matusi yanakuja. 4 Maneno ya kinywa cha mutu ni kilindi cha maji; chemichemi ya hekima ni kijito kinachobubujika. 5 Si vizuri kumupendelea mutu mwovu, na kumunyima sheria mutu wa haki. 6 Maneno ya mupumbafu yanaleta ugomvi; kila neno analosema linasababisha azabu. 7 Kinywa cha mupumbafu kinamwangamiza mwenyewe; mudomo wake ni mutego wa kumunasa yeye mwenyewe. 8 Maneno ya muchongeaji ni kama chakula kitamu ambacho kinashuka mpaka ndani kabisa ya tumbo. 9 Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu. 10 Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama. 11 Tajiri anazani kwamba mali ni makimbilio yake; anafikiri hayo ni ukuta murefu unaomulinda. 12 Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima. 13 Kujibu mbele ya kusikiliza ni upumbafu na jambo la haya. 14 Roho ya mutu inaweza kuvumilia ugonjwa, lakini ukiwa umevunjika moyo, utavumilia namna gani? 15 Mutu mwenye akili anajipatia maarifa; sikio la mwenye hekima linatafuta maarifa. 16 Zawadi inamufungulia mutu milango; inaweza kumufikisha mutu mbele ya mukubwa. 17 Anayejitetea wa kwanza anaonekana kuwa na haki, mpaka pale mupinzani wake atakapoanza kumupinga. 18 Kura inakomesha ubishi; inaamua kati ya wakubwa wanaopingana. 19 Ndugu aliyetendewa kosa ni mugumu kuliko muji wenye ukuta; magomvi yanakaza kama vile vifungio vya mulango wa ukuta. 20 Maneno ya mutu yanaweza kumushibisha; anatosheka kwa matokeo ya maneno yake. 21 Ulimi una nguvu ya kuleta uzima na kuua; wanaopenda kuutumia watakula matunda yake. 22 Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe. 23 Masikini anaomba kwa unyenyekevu, lakini tajiri anajibu kwa ukali. 24 Warafiki wengi wanaweza kumwangusha mutu, lakini kuna rafiki mwaminifu kuliko ndugu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo