Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mezali 15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kujibu kwa upole kunatuliza hasira, lakini neno kali linachochea hasira.

2 Ulimi wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini watu wapumbafu wanamwanga maneno ya ujinga.

3 Macho ya Yawe yanaona kila kitu, yanachunguza kibaya na kizuri.

4 Ulimi mupole ni musingi wa uzima, lakini uovu wake unavunja moyo.

5 Mupumbafu anazarau mafundisho ya baba yake, lakini anayekubali maonyo ni mwenye akili.

6 Katika nyumba ya mwenye haki kuna wingi wa mali, lakini mapato ya waovu yanaleta hasara.

7 Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.

8 Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.

9 Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini Mungu anawapenda wale wanaofuata mambo ya haki.

10 Azabu kali ni kwa wanaoacha mwenendo mwema; yeyote anayechukia kuonywa atakufa.

11 Ikiwa Yawe anajua kuzimu na shimo la kuangamia, mawazo ya mwanadamu yataweza namna gani kujificha mbele yake?

12 Mwenye mazarau hapendi kuonywa, hatafuti hata kidogo maoni ya wenye hekima.

13 Moyo wa furaha unaangarisha uso, lakini uchungu unavunja moyo.

14 Mwenye akili anatafuta maarifa, lakini wapumbafu wanajikulisha upumbafu.

15 Kwa mwenye kuteswa, kila siku ni mbaya, lakini kwa mwenye raha ni sikukuu.

16 Afazali kuwa na kidogo na kumwogopa Yawe, kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.

17 Afazali kula mboga za majani kwa upendo, kuliko karamu ya nyama nono pamoja na chuki.

18 Mutu wa hasira mbaya anasababisha ugomvi, lakini asiyekuwa mwepesi wa hasira anautuliza.

19 Njia ya muvivu inajaa miiba, lakini njia ya mutu wa usawa ni wazi kama barabara kubwa.

20 Mutoto mwenye hekima anamufurahisha baba yake, lakini mupumbafu anamuzarau mama yake.

21 Upumbafu ni furaha kwa mutu asiyekuwa na akili, lakini mwenye akili anachagua njia inayokuwa sawa.

22 Mipango inaharibika kwa kukosa shauri, lakini kwa washauri wengi, inasimama.

23 Kutoa jibu zuri kunafurahisha; neno linalofaa kwa wakati wake ni jema sana!

24 Njia ya mwenye hekima inaelekea juu kwenye uzima, kusudi aepuke kuingia chini katika kuzimu.

25 Yawe anabomoa makao ya wenye kiburi, lakini analinda mipaka ya makao ya mujane.

26 Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maneno mema yanamufurahisha.

27 Anayetamani faida ya unyanganyi anataabisha jamaa yake, lakini anayechukia kituliro ataishi.

28 Moyo wa mwenye haki unafikiri mbele ya kujibu, lakini kinywa cha mwovu kinatapika uovu.

29 Yawe anajiweka mbali na watu waovu, lakini yuko karibu na wenye haki kwa kuwasikiliza.

30 Uso wenye kuangaa unafurahisha moyo. Habari njema inarudishia mwili nguvu.

31 Mutu ambaye anasikiliza maonyo mema ana nafasi yake kati ya wenye hekima.

32 Anayekataa kufundishwa anajizarau mwenyewe, lakini anayekubali maonyo anapata ufahamu.

33 Kumwogopa Yawe ni mafundisho ya hekima; mbele ya kuheshimika inafaa kuwa munyenyekevu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan