Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Mezali 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.

2 Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.

3 Mutu hawezi kudumu katika kutenda maovu, lakini hakuna kitu kinachoweza kumwangusha mutu wa haki.

4 Muke mwema ni taji la utukufu kwa mume wake. Anayemupatisha mume wake haya ni kama kidonda ndani ya mifupa yake.

5 Mawazo ya mwenye haki ni ya haki; mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.

6 Maneno ya waovu shabaha yake ni kuua, lakini kinywa cha mutu wa usawa kinaokoa.

7 Waovu wanaangamizwa na kutoweka kabisa, lakini jamaa ya wenye haki itasimama.

8 Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.

9 Afazali mutu wa chini anayejitegemea kuliko yule anayejitakia makubwa na kukosa chakula.

10 Mutu mwenye haki anajali nyama wake, lakini huruma za waovu ni kutesa tu.

11 Mulimaji mwenye bidii ana chakula tele, lakini anayefuata mambo yasiyofaa hana akili.

12 Matumaini ya waovu yanaporomoka na kuharibika, lakini mutu mwenye haki anasimama imara.

13 Mutu mwovu ananaswa kwa uongo wake mwenyewe, lakini mwenye haki anatoka katika taabu.

14 Mutu anafanikiwa kutokana na maneno yake kama vile anavyopata matokeo ya kazi za mikono yake.

15 Mupumbafu anaona njia yake kuwa sawa, lakini mwenye hekima anasikiliza shauri.

16 Ujinga wa mupumbafu unajulikana mara moja, lakini mwerevu anazarau matusi.

17 Musema kweli anatoa ushuhuda wa kweli, lakini mushuhuda wa uongo anasema udanganyifu.

18 Maneno ya ovyo yanaumiza kama upanga, lakini kusema kwa mwenye hekima kunaponyesha kidonda.

19 Ukweli unadumu milele, lakini uongo ni wa muda kidogo tu.

20 Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu ndani ya moyo, lakini wanaokusudia mema wana furaha.

21 Wenye haki hawapatwi na jambo lolote baya, lakini waovu wanapata hasara nyingi.

22 Kinywa kinachosema uongo ni chukizo kwa Yawe, lakini watu waaminifu ni furaha yake.

23 Mutu mwerevu anaficha maarifa yake, lakini wapumbafu wanatangaza upumbafu wao.

24 Kuwa na bidii kutamupa mutu cheo, lakini uvivu utamufanya mutumwa.

25 Wasiwasi ndani ya moyo inamukosesha mutu raha, lakini neno zuri linamuchangamusha.

26 Mutu wa haki anaepuka uovu, lakini njia ya waovu inawapotosha wenyewe.

27 Mwindaji muvivu hatapata anachowinda, lakini mwenye bidii atafanikiwa.

28 Haki ni njia ya uzima, lakini uovu unaongoza katika kifo.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan