Matayo 19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mafundisho ya Yesu juu ya kuvunja ndoa ( Mk 10.1-12 ) 1 Yesu alipomaliza kusema maneno hayo akaondoka Galilaya. Akaenda katika jimbo la Yudea na kuvuka ngambo ya Yordani. 2 Na makundi mengi ya watu wakamufuata, naye akawaponyesha wagonjwa kule. 3 Wafarisayo wamoja wakamufikia kwa kumupima, wakamwuliza: “Sheria yetu inamuruhusu mutu kumufukuza muke wake haizuru kwa sababu gani?” 4 Yesu akajibu: “Hamujasoma bado maneno yanayoandikwa katika Maandiko Matakatifu? ‘Kwa mwanzo Muumba aliumba mwanaume na mwanamuke,’ 5 na kisha akasema: ‘Kwa sababu hii, mutu atawaacha baba yake na mama yake na kuungana na muke wake, nao wawili watakuwa mwili mumoja.’ 6 Hivi wao si wawili tena, lakini wanakuwa mumoja. Basi mutu asitenganishe kile Mungu alichokiunganisha.” 7 Halafu Wafarisayo wakamwuliza: “Kwa sababu gani basi Musa aliamuru kuandika barua ya kuachana wakati wa kumufukuza mwanamuke?” 8 Yesu akawajibu: “Musa aliwapa ninyi ruhusa ya kuachana na wake wenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini haikuamuriwa vile tangu mwanzo. 9 Na sasa mimi ninawaambia: kila mutu anayeachana na muke wake, isipokuwa kwa sababu ya uzinzi tu, na kumwoa muke mwingine, anazini.” 10 Wanafunzi wake wakamwambia: “Ikiwa hayo ndiyo mapaswa ya mume kwa muke, hakuna mafaa ya kuoa.” 11 Yesu akawajibu: “Si watu wote wanaoweza kukubali neno hilo munalosema, isipokuwa tu wale wanaojaliwa na Mungu. 12 Kulingana na hayo, watu wamoja hawawezi kuoa kwa sababu walizaliwa towashi, wengine wamefanywa kuwa towashi na watu, wengine wamejifanya vile wenyewe kwa sababu ya kutumikia Ufalme wa mbinguni. Anayeweza kukubali mafundisho haya, ayakubali!” Yesu anabariki watoto ( Mk 10.13-16 ; Lk 18.15-17 ) 13 Watu wamoja walimuletea Yesu watoto kusudi awawekee mikono na kuwaombea, lakini wanafunzi wakawakaripia watu wale. 14 Lakini Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.” 15 Naye alipokwisha kuweka mikono juu yao, akaondoka pale. Kijana aliyekuwa tajiri ( Mk 10.17-31 ; Lk 18.18-30 ) 16 Kijana mumoja akamufikia Yesu na kumwuliza: “Mwalimu, nifanye jambo gani jema kusudi nipate uzima wa milele?” 17 Yesu akamujibu: “Sababu gani unaniuliza juu ya jambo linalokuwa jema? Kuna mumoja tu anayekuwa mwema. Kama ukitaka kuingia pahali utakapopata uzima wa kweli, utii amri za Mungu.” 18 Naye akauliza: “Amri gani?” Yesu akamujibu: “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, 19 uwaheshimu baba yako na mama yako na kumupenda mwenzako sawa wewe mwenyewe.” 20 Yule kijana akamwambia: “Nimetii hizo amri zote. Ninakosewa na nini tena?” 21 Yesu akamujibu: “Ukitaka kuwa mutimilifu, kwenda uuzishe vitu unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate.” 22 Lakini yule kijana aliposikia maneno hayo, akajiendea akihuzunika, kwa sababu alikuwa tajiri sana. 23 Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kweli ninawaambia: ni vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni. 24 Ninawaambia tena: ni kwepesi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.” 25 Wanafunzi waliposikia maneno haya, wakashangaa sana na kuuliza: “Ni nani basi anayeweza kuokolewa?” 26 Yesu akawaangalia na kuwaambia: “Jambo hilo haliwezi kutendeka kwa uwezo wa mwanadamu, lakini kwa uwezo wa Mungu, yote yanawezekana.” 27 Halafu Petro akamwuliza: “Angalia, sisi tumeacha vyote na kukufuata wewe! Basi na sisi tutapata nini?” 28 Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: Katika ulimwengu mupya, Mwana wa Mutu atakapoikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu, ninyi kumi na wawili mulionifuata mutaikaa vilevile juu ya viti kumi na viwili vya kifalme kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli. 29 Na kila mutu aliyeacha nyumba yake, kaka, dada, baba, mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara nyingi zaidi na kupewa uzima wa milele. 30 Lakini wengi wanaokuwa wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wengi wanaokuwa wa mwisho watakuwa wa kwanza. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo