Matayo 18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Ni nani anayekuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni ( Mk 9.33-37 ; Lk 9.46-48 ) 1 Wakati ule wanafunzi wakamufikia Yesu, wakamwuliza: “Ni nani anayekuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni?” 2 Halafu akamwita mutoto mudogo, akamusimamisha katikati yao 3 na kusema: “Kweli ninawaambia: kama musipogeuka na kuwa sawasawa na mutoto mudogo, hamutaingia katika Ufalme wa mbinguni hata kidogo. 4 Basi kila mutu atakayekuwa munyenyekevu kama huyu mutoto mudogo, ndiye atakayekuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni. 5 Naye anayemupokea mutoto mudogo kama huyu kwa ajili ya jina langu, ananipokea mimi. Hatari ya zambi ( Mk 9.42-48 ; Lk 17.1-2 ) 6 “Lakini anayeangusha mumoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingalikuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kuzamishwa ndani ya bahari. 7 Ole kwa dunia kwa ajili ya vikwazo vinavyokuwa ndani yake! Vikwazo haviwezi kosa kutokea, lakini ole kwa mutu yule anayevileta! 8 “Kama mukono wako au muguu wako ukikukosesha, uukate na kuutupa mbali! Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukikuwa na mukono mumoja au ukikuwa kilema. Hiyo ni vizuri kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili na kutupwa katika moto kwa milele. 9 Na kama jicho lako likikukosesha, uliongoe na kulitupa mbali! Ni heri kwako kuingia pahali utakapopata uzima wa kweli ukikuwa na jicho moja kuliko kuwa na macho mawili na kutupwa katika moto wa jehenamu. Mufano wa kondoo aliyapotea ( Lk 15.3-7 ) 10 “Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [ 11 Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kuokoa yule aliyepotea.] 12 “Munafikiri nini? Kama mutu akiwa na kondoo mia moja, na mumoja wao akipotea, hatawaacha wale wengine makumi tisa na tisa juu ya mulima na kwenda kumutafuta yule aliyepotea? 13 Na kama akimupata yule kondoo, kweli ninawaambia, anamufurahia kuliko wale makumi tisa na tisa waliobaki bila kupotea. 14 Ni hivi vilevile Baba yenu anayekuwa mbinguni hataki hata mumoja wa hawa wadogo kupotea. Kuonya ndugu anayekosa 15 “Kama ndugu yako akikukosea, umwendee kwa kumwonyesha kosa lake, mukiwa ninyi wawili peke yenu. Na kama akikusikia, unarudiliana na ndugu yako. 16 Lakini kama akikataa kukusikia, utwae mutu mumoja au wawili na kumwendea pamoja nao, kusudi kila neno lihakikishwe kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu, sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema. 17 Na kama akikataa kuwasikia watu wale, upeleke habari kwa kanisa. Naye akikataa kusikia kanisa vilevile, umuhesabu kama mupagani na mutenda maovu sawa walipishaji wa kodi. Kukataza na kuruhusu 18 “Hivi, kweli ninawaambia: chochote mutakachokikataza katika dunia kitakatazwa mbinguni vilevile, na chochote mutakachokiruhusu katika dunia, kitaruhusiwa mbinguni vilevile. 19 “Kweli ninawaambia tena: wawili kati yenu hapa katika dunia wakipatana kwa kuomba juu ya kitu chochote, Baba yangu anayekuwa mbinguni atawapa kitu kile. 20 Kwa maana pahali popote watu wawili au watatu wanapokusanyika kwa ajili ya jina langu, mimi ni pale katikati yao.” Mufano wa mutumishi aliyekataa kusamehe 21 Kisha Petro akamwendea Yesu na kumwuliza: “Bwana, ndugu yangu akiendelea kunikosea, nitamusamehe mpaka mara ngapi? Mara saba inatosha?” 22 Yesu akamujibu: “Hapana, sikuambii kwamba umusamehe mara saba tu, lakini mpaka mara makumi saba mara saba. 23 Ni kwa sababu hii Ufalme wa mbinguni unafanana na mufalme mumoja aliyetaka kufanya hesabu ya madeni watumishi wake waliyokuwa nayo. 24 Alipoanza kufanya hesabu ile, wakamuletea mutumishi mumoja aliyekuwa na deni lake la mamilioni ya feza. 25 Na kwa kuona mutumishi yule hakukuwa na jinsi ya kulipa deni lile, bwana wake akaamuru auzishwe kuwa mutumwa, yeye na muke wake pamoja na watoto wake na vyote alivyokuwa navyo viuzishwe vilevile, kusudi apate kumulipa. 26 Basi mutumishi yule akamupigia bwana wake magoti, akamusihi, akisema: ‘Ninakuomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote!’ 27 Yule bwana akamusikilia mutumishi yule huruma, akamusamehe deni lile na kumwacha kwenda. 28 “Mutumishi yule alipoondoka, akakutana na mumoja wa watumishi wenzake aliyekuwa na deni lake la vikoroti mia moja vya feza. Akamukamata na kumunyonganyonga shingo na kumulazimisha kulipa deni lake. 29 Huyo mutumishi mwenzake akamupigia magoti na kumusihi, akisema: ‘Ninakuomba univumilie, nami nitakulipa deni lako!’ 30 Lakini hakutaka, akamupeleka katika kifungo mpaka atakapolipa deni lile. 31 Nao watumishi wenzake walipoona jambo hilo, wakahuzunika sana, wakaenda kumwelezea bwana wao yote yaliyotokea. 32 Halafu yule bwana akamwita mutumishi yule na kumwambia: ‘Wewe ni mutumishi mubaya! Mimi nilikusamehe deni lako lote, kwa sababu ulinisihi. 33 Wewe vilevile ulipaswa kumuhurumia mutumishi mwenzako sawa vile mimi nilivyokuhurumia.’ 34 Basi yule bwana akakasirika sana, akamutoa mutumishi yule aazibiwe mpaka atakapolipa lile deni lake.” 35 Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi vilevile Baba yangu anayekuwa mbinguni atakavyowatendea ninyi, kama kila mumoja wenu asipomusamehe ndugu yake kwa moyo wake wote.” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo