Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Marko 11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Yesu anaingia Yerusalema
( Mat 21.1-11 ; Lk 19.28-40 ; Yn 12.12-19 )

1 Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema, upande wa kijiji cha Betefage na cha Betania, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili katika wanafunzi wake,

2 akiwaambia: “Mwende katika kijiji kinachokuwa mbele yenu. Wakati mutakapofika kule, mutaona mwana-punda amefungwa, na hakuna mutu aliyekwisha kupanda juu yake. Mumufungue na kumuleta hapa.

3 Na kama mutu akiwauliza: ‘Kwa sababu gani munafanya hivi? Mumwambie kwamba Bwana yuko na lazima ya kumutumia, atamurudisha hapa nyuma kidogo.’ ”

4 Basi wakaenda, wakaona mwana-punda amefungwa inje, karibu na mulango wa nyumba pembeni ya barabara. Walipokuwa wakimufungua,

5 watu waliokuwa pale wakawauliza: “Munafanya nini? Kwa nini munamufungua mwana-punda huyu?”

6 Wakawajibu sawa vile Yesu alivyowaambia, nao watu wale wakawaruhusu kwenda.

7 Wakamuletea Yesu yule mwana-punda na kutandika nguo zao juu yake. Kisha Yesu akaikaa juu yake.

8 Watu wengi wakatandika nguo zao katika njia na wengine wakatandika matawi waliyokata katika mashamba.

9 Watu waliotangulia mbele ya Yesu na wale waliofuata nyuma yake wakaanza kulalamika kwa sauti kubwa, wakisema: “Mungu asifiwe! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana!

10 Ubarikiwe ufalme unaokuja, ndio ufalme wa babu yetu Daudi! Mungu asifiwe juu mbinguni!”

11 Yesu akafika Yerusalema na kuingia ndani ya hekalu. Alipokwisha kuangalia vitu vyote pande zote, akaondoka na kwenda Betania pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili, kwa sababu ilikuwa imekwisha kuwa magaribi.


Yesu analaani muti was matunda ya tini
( Mat 21.18-19 )

12 Kesho yake, walipotoka Betania, Yesu akasikia njaa.

13 Akaona kwa mbali muti wa tini wenye majani mengi. Basi akaenda kuangalia kama atapata matunda juu ya muti ule. Lakini alipofika karibu nao, hakuona kitu juu yake isipokuwa majani matupu, kwa sababu haikukuwa wakati wake wa kutoa matunda.

14 Halafu Yesu akalaani muti ule, akisema: “Tangia sasa hata milele, mutu asipate tena tunda tokea juu yako.” Nao wanafunzi wake wakasikia maneno hayo aliyosema.


Yesu anafukuza wachuuzi katika hekalu
( Mat 21.12-17 ; Lk 19.45-48 ; Yn 2.13-22 )

15 Kisha wakafika Yerusalema. Yesu alipoingia ndani ya hekalu, akaanza kufukuza watu waliokuwa wakiuzishia na kununulia vitu vyao ndani ya hekalu. Akapindua meza za wale waliobadilisha feza na viti vya wachuuzi wa njiwa.

16 Vilevile akawakataza watu kukatiliza na mizigo yao katika kiwanja cha hekalu.

17 Kisha akawafundisha maneno haya: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi kwa mataifa yote.’ Lakini ninyi mumeigeuza kuwa nafasi ya kukutania ya wanyanganyi!”

18 Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walipopata habari hii, wakatafuta njia ya kumwua Yesu. Lakini walimwogopa, kwa sababu kundi lote la watu walishangaa na mafundisho yake.

19 Ilipokuwa magaribi, Yesu na wanafunzi wake wakatoka katika muji ule.


Mafundisho kutoka muti wa tini uliolaaniwa
( Mat 21.20-22 )

20 Kesho yake asubui, walipokuwa wakipita, wakaona ule muti wa tini, nao ulikuwa umekauka wote, hata mizizi yake.

21 Petro akakumbuka mambo yaliyotokea mbele, akamwambia Yesu: “Mwalimu, angalia, ule muti wa tini ulioulaani umekauka.”

22 Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Mumwamini Mungu.

23 Kweli ninawaambia: ‘Mutu anaweza kuuambia mulima huu kwamba uondoke hapa na kujitupa katika bahari.’ Na ikiwa anasema maneno yale bila shaka katika moyo wake, lakini akiamini kama jambo lile litafanyika, hakika litafanyika kwake.

24 Ni kwa hiyo ninawaambia kwamba munapoomba kwa ajili ya hitaji la kitu fulani, mwamini kama mumekwisha kukipokea, na kwa njia hiyo mutakipewa.

25 Na munaposimama kwa kuomba, mukiwa na neno na mutu mwingine, mumusamehe, kusudi Baba yenu anayekuwa mbinguni, awasamehe vilevile makosa yenu. [

26 Lakini musipowasamehe wengine, Baba yenu anayekuwa mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu vilevile.]”


Mamlaka ya Yesu yanatoka wapi?
( Mat 21.23-27 ; Lk 20.1-8 )

27 Yesu na wanafunzi wake wakafika tena Yerusalema. Yesu alipokuwa akitembea katika hekalu, wakubwa wa makuhani, walimu wa Sheria pamoja na wasimamizi wa watu, wakamufikia.

28 Wakamwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka haya?”

29 Yesu akawajibu: “Nitawauliza ulizo moja tu. Kama mukinijibu, mimi vilevile nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.

30 Yoane alipata mamlaka ya kubatiza kutoka kwa nani? Kwa Mungu au kwa watu? Munijibu.”

31 Nao wakaanza kupiga mafikiri pamoja na kusema: “Kama tukijibu kwamba mamlaka yake yalitoka kwa Mungu, atatuuliza: ‘Kwa sababu gani hamukumwamini?’

32 Vilevile hatuwezi kusema kama yalitoka kwa watu…” (Waliogopa kundi la watu kwa maana wote walisadiki kama Yoane alikuwa nabii wa kweli).

33 Basi wakamujibu Yesu: “Hatujui.” Naye akawaambia: “Nami vilevile sitawaambia ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan