Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Malaki 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Watu si waaminifu kwa Mungu

1 Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.

2 Lakini ni nani atakayevumilia siku ile atakapokuja? Ni nani atakayesimama kuvumilia atakapotokea? Yeye ni kama moto mukali unaosafisha chuma; ni kama sabuni ya mwenye kufua nguo.

3 Yeye atakuja kuhukumu kama mutu anayesafisha na kutakasa feza. Atawasafisha wazao wa Lawi, kama mutu anavyofua zahabu au feza, mpaka wamutolee Yawe sadaka zinazokubalika.

4 Hivyo, sadaka za watu wa Yuda na wa Yerusalema zitamupendeza Yawe kama za watu wa zamani; kama katika miaka iliyopita.

5 Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Zaka na sadaka

6 Yawe wa majeshi alisema hivi: Mimi Yawe sibadiliki. Ni kwa sababu hii, ee ninyi wazao wa Yakobo, hamujateketezwa.

7 Tangu wakati wa babu zenu, mumeyazarau masharti yangu wala hamukuyafuata. Munirudilie, nami nitawageukia. Lakini ninyi munaniuliza: Tutakurudilia namna gani?

8 Ninawajibia hivi: Ni sawa kwa mutu kumudanganya Mungu? Hapana! Lakini ninyi munanidanganya! Ingawa hivyo ninyi munauliza: Tunakudanganya kwa namna gani? Kweli! Munanidanganya juu ya zaka na sadaka zenu.

9 Ninyi na taifa lenu lote mumelaaniwa kwa sababu ya kunidanganya.

10 Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.

11 Wadudu waharibifu nitawazuia wasiyaharibu tena mazao yenu. Mizabibu yenu katika mashamba haitaacha kuzaa matunda.

12 Halafu mataifa yote yatawaita ninyi watu waliobarikiwa, maana inchi yenu itakuwa inchi ya furaha. –Ni Yawe, Mungu Mukubwa anayesema hivyo.

13 Yawe anasema hivi: Maneno yenu yamekuwa muzigo kwangu. Hata hivyo munasema: Tumesema nini juu yako?

14 Ninyi mumesema: Kumutumikia Mungu hakuna faida. Kuna faida gani kuyatii maagizo ya Yawe wa majeshi, au kujaribu kumwonyesha kwamba tumekosa mbele yake kwa kutembea kama watu wanaoomboleza?

15 Tunayoona sisi, ni kwamba wenye kiburi ndio wenye furaha siku zote. Watu waovu, ingawa wanastawi, hata wanapomujaribu Mungu, hawapati azabu.

16 Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.

17 Kisha Yawe wa majeshi akasema hivi: Hao watakuwa watu wangu. Watakuwa urizi wangu wa kipekee siku ile nitakaposimama kufanya jambo ninalokusudia. Sitawazuru kama vile baba asivyomuzuru mwana wake anayemutumikia.

18 Pale ndipo mutakapotambua tena tofauti inayokuwa kati ya wenye haki na waovu, kati ya mutu anayemutumikia Mungu na asiyemutumikia.


Siku ya Yawe inakuja

19 Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku inakuja, nayo inawaka kama furu. Wenye kiburi na waovu wote watatupwa mule na kuteketezwa kama majani yenye kukauka; watateketea kabisa wala hakutabaki hata kitambulisho.

20 Lakini kwa ajili yenu ninyi munaonitii, uwezo wangu wa kuokoa utawatokea kama jua linalokuwa na nguvu za uponyaji kwenye mishale yake. Mutatoka mukirukaruka kama wana-ngombe wanapotoka katika zizi lao.

21 Siku hiyo mutawakanyagakanyaga waovu, nao watakuwa kama majivu chini ya miguu yenu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.

22 Mukumbuke sheria, masharti na maagizo yangu niliyomwamuru mutumishi wangu Musa kwenye mulima Horebu, kusudi awaamuru watu wote wa Israeli.

23 Mbele ya kufika kwa siku ile kubwa na ya kutisha, nitamutuma nabii Elia.

24 Nabii Elia atawapatanisha wazazi na watoto wao; kama sivyo, nitakuja na kuiangamiza inchi yenu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan