Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Luka 4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kujaribiwa kwa Yesu
( Mat 4.1-11 ; Mk 1.12-13 )

1 Yesu, akarudia toka kwenye muto Yordani, akijazwa na Roho, na Roho huyo akamwongoza kwenda katika jangwa.

2 Kule akajaribiwa na Shetani kwa muda wa siku makumi ine. Kwa muda ule, yeye hakukula kitu. Na wakati siku zile zilipotimia, akasikia njaa.

3 Halafu Shetani akamufikia na kumwambia: “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili ligeuke mukate.”

4 Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Mutu hawezi kuishi kwa mukate tu.’ ”

5 Kisha Shetani akamupeleka kwenye nafasi inayoinuka juu sana. Akamwonyesha mara moja falme zote za dunia,

6 na kumwambia: “Nitakupa falme hizo zote zenye uwezo na utukufu, kwa maana mimi nimezipewa zote, nami ninaweza kuzitoa kwa mutu yeyote ninayetaka.

7 Basi ukiinama mbele yangu kwa kuniabudu, zote zitakuwa zako.”

8 Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”

9 Halafu Shetani akamupeleka Yerusalema. Akamusimamisha juu sana kwenye pembe la hekalu na kumwambia: “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, ujitupe chini,

10 kwa maana inaandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Mungu atawaamuru wamalaika wake wakulinde.

11 Watakubeba katika mikono yao, kusudi muguu wako usijikwae juu ya jiwe.’ ”

12 Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Usimujaribu Bwana Mungu wako.’ ”

13 Shetani alipokwisha kumujaribu Yesu namna zote, akamwacha kwa muda.


Yesu anaanza kazi yake katika Galilaya
( Mat 4.12-17 ; Mk 1.14-15 )

14 Yesu akarudia Galilaya akijazwa na uwezo wa Roho, na habari zake zikaenea fasi zote katika pande zile.

15 Alifundisha katika nyumba zao za kuabudia, na kusifiwa na watu wote.


Yesu anakataliwa Nazareti
( Mat 13.53-58 ; Mk 6.1-6 )

16 Yesu akafika Nazareti, nafasi alipokomalia. Siku ya Sabato ilipotimia akaingia katika nyumba ya kuabudia kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama kwa kusoma Maandiko Matakatifu;

17 wakamupa kitabu cha nabii Isaya. Halafu akakifungua na kupata nafasi inayoandikwa:

18 “Roho wa Bwana yuko pamoja nami, maana amenichagua niwahubirie wamasikini Habari Njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kwamba watakombolewa nao vipofu kwamba wataona. Amenituma kuwapa wanaoteswa uhuru,

19 na kutangaza mwaka ambao Bwana atawajalia watu neema.”

20 Kisha akafunga kile kitabu, akakipatia mutumishi wa nyumba ya kuabudia na kuikaa. Na watu wote waliokuwa ndani ya ile nyumba ya kuabudia wakamukazia macho.

21 Halafu akaanza kuwaambia: “Maandiko haya yametimia leo.”

22 Nao wote wakamufurahia na kushangaa na maneno mazuri aliyosema. Wakasema: “Huyu si mwana wa Yosefu?”

23 Yesu akawaambia: “Hakika mutaniambia fumbo hili: ‘Muganga, ujiponyeshe wewe mwenyewe!’ Na vilevile mutaniambia hivi: ‘Tumesikia mambo yote uliyotenda katika muji Kapernaumu, basi uyafanye hapa vilevile katika muji wako.’ ”

24 Naye akaongeza kusema: “Kweli ninawaambia: hakuna nabii anayekubaliwa katika muji wake.

25 Ninawaambia ukweli: kulikuwa wajane wengi katika inchi ya Israeli katika siku za nabii Elia. Wakati ule, mvua ilifungwa isinyeshe kwa muda wa miaka mitatu na nusu na kukakuwa njaa kubwa katika inchi yote.

26 Lakini Elia hakutumwa kwa mutu yeyote kati yao, isipokuwa tu kwa yule mujane wa Zarepata, katika inchi ya Sidona.

27 Vilevile kulikuwa watu wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna mumoja kati yao aliyetakaswa, isipokuwa tu Namani wa inchi ya Suria.”

28 Watu wote waliokuwa ndani ya ile nyumba ya kuabudia, wakakasirika sana wakati waliposikia maneno hayo.

29 Wakasimama, wakamusukuma Yesu hata inje ya muji wao, uliojengwa juu ya kilima. Wakamupeleka kwenye maporomoko kusudi wamutupe chini.

30 Lakini yeye akapita katikati yao, na kujiendea.


Mutu aliyeshikwa na pepo
( Mk 1.21-28 )

31 Halafu Yesu akaenda Kapernaumu, katika jimbo la Galilaya. Siku ya Sabato ilipotimia, akawafundisha watu.

32 Nao wakashangaa sana kuona namna alivyowafundisha, kwa maana aliwafundisha kama mutu mwenye mamlaka.

33 Na ndani ya nyumba ya kuabudia kulikuwa mutu aliyeshikwa na pepo. Naye alilalamika kwa sauti kubwa,

34 akisema: “Ee Yesu wa Nazareti, kuna maneno gani kati yako na sisi? Ulikuja kutuangamiza? Ninakutambua wewe ni nani. Wewe ni Mutakatifu wa Mungu.”

35 Yesu akamukaripia, akimwamuru hivi: “Nyamaza, na utoke ndani ya mutu huyu!” Na yule pepo akamutupa yule mutu chini mbele ya watu, na kutoka ndani yake pasipo kumwumiza.

36 Watu wote wakashangaa sana na kusemezana: “Hatujaona mambo kama haya! Mutu huyu anawaamuru pepo kwa mamlaka na uwezo wake, nao wanatoka!”

37 Na habari za Yesu zikaenea katika jimbo lile lote.


Yesu anawaponyesha wagonjwa wengi
( Mat 8.14-17 ; Mk 1.29-34 )

38 Yesu akatoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, akaenda kwa nyumba ya Simoni. Mama mukwe wa Simoni alikuwa ameshikwa na homa kali, halafu wakamwomba Yesu amuponyeshe.

39 Basi akainama kunapokuwa yule mama, akaamuru ile homa itoke ndani yake, naye akapona. Na mara moja akasimama na kuanza kuwashugulikia.

40 Jua lilipotua, wakamuletea Yesu watu wote wenye kuwa na magonjwa mbalimbali. Akaweka mikono yake juu ya kila mumoja wao, akawaponyesha.

41 Pepo wakatoka ndani ya watu wengi, wakilalamika, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakaripia, na hakuwaachilia waseme neno, kwa sababu walijua kwamba yeye ndiye Kristo.


Yesu anahubiri katika Yudea
( Mk 1.35-39 )

42 Kulipokucha kesho yake, Yesu akatoka katika muji na kwenda pahali penye ukiwa. Kundi kubwa la watu wakaanza kumutafuta. Nao walipomwona walitaka kumuzuia kusudi asitoke kwao.

43 Lakini Yesu akawaambia: “Imenipasa kuhubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu katika miji mingine vilevile, kwa maana ni kwa sababu ile nimetumwa.”

44 Naye akaendelea kuhubiri katika Yudea ndani ya nyumba za kuabudia.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan