Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Luka 18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mufano wa mujane na mwamuzi

1 Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu kwa kuwaonyesha kwamba wanapaswa kuomba siku zote pasipo kuchoka.

2 Akasema: “Katika muji mumoja, kulikuwa mwamuzi mumoja asiyemwogopa Mungu wala kumujali na mutu yeyote.

3 Vilevile katika muji ule, kulikuwa mujane mumoja aliyekuwa akimwendea yule mwamuzi akimusihi: ‘Unipatie haki yangu juu ya mupinzani wangu.’

4 Kwa muda murefu yule mwamuzi alikataa. Lakini kisha akajiuliza mwenyewe: ‘Ijapokuwa mimi simwogopi Mungu wala simujali mutu yeyote,

5 lakini kwa sababu mujane huyu anazidi kuniuzi nitamupatia haki yake, kusudi asiendelee kufika hapa na kunikasirikisha.’ ”

6 Halafu Bwana akasema: “Musikilize jinsi mwamuzi huyu mubaya anavyosema!

7 Basi, Mungu hatawapatia haki wale wachaguliwa wake wanaomulilia usiku na muchana? Au atakawia kuwasaidia?

8 Ninawaambia ninyi: hatakawia kuwapatia haki. Lakini Mwana wa Mutu atakaporudia, atakuta watu wenye kumwamini katika dunia?”


Mufano wa Mufarisayo na mulipishaji wa kodi

9 Vilevile Yesu akawaambia mufano huu kwa ajili ya watu waliojiona kuwa wenye haki na kuwazarau wengine.

10 “Siku moja watu wawili walienda kuomba kwenye hekalu; mumoja alikuwa Mufarisayo na mwingine alikuwa mulipishaji wa kodi.

11 Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.

12 Ninafunga kula chakula mara mbili kila juma na ninatoa fungu moja la kumi la vitu vyote ninavyopata.’

13 Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”

14 Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Yesu anabariki watoto wadogo
( Mat 19.13-15 ; Mk 10.13-16 )

15 Watu wamoja walimuletea Yesu hata watoto wadogo kusudi awaguse. Wanafunzi walipoona vile, wakawakaripia watu wale.

16 Lakini Yesu akawaita na kusema: “Muwaache watoto wadogo wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.

17 Kweli ninawaambia: ‘Mutu yeyote asiyekubali Ufalme wa Mungu kama mutoto mudogo, hawezi kuingia katika Ufalme ule hata kidogo.’ ”


Kijana tajiri
( Mat 19.16-30 ; Mk 10.17-31 )

18 Mutawala mumoja akamwuliza Yesu: “Mwalimu mwema, nifanye nini kusudi nipate uzima wa milele?”

19 Yesu akamwuliza: “Sababu gani unaniita mwema? Hakuna mutu anayekuwa mwema isipokuwa Mungu peke yake.

20 Unajua jinsi amri zinavyosema kwamba: ‘Usizini, usiue, usiibe, usishuhudie uongo, uwaheshimu baba yako na mama yako.’ ”

21 Yule mutu akamujibu: “Nimetii amri zile zote tangu ujana wangu.”

22 Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”

23 Lakini mutu yule aliposikia maneno yale, akahuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.

24 Yesu alipoona kwamba amehuzunika sana, akasema: “Kweli ni vigumu sana kwa watajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu,

25 lakini ni kwepesi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

26 Nao waliosikia maneno haya wakasema: “Ni nani basi anayeweza kuokolewa?”

27 Yesu akajibu: “Mambo yasiyoweza kutendeka kwa uwezo wa mwanadamu yanawezekana kwa Mungu.”

28 Basi Petro akamwambia: “Sisi tumeacha vyote tulivyokuwa navyo na kukufuata wewe!”

29 Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: kama mutu akiacha nyumba yake, muke, wandugu, wazazi, au watoto wake kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,

30 atapokea mara mingi zaidi katika wakati wa sasa. Na katika wakati utakaokuja atapokea uzima wa milele.”


Yesu anajulisha mara tatu habari za kufa na kufufuka kwake
( Mat 20.17-19 ; Mk 10.32-34 )

31 Halafu Yesu akawatwaa wanafunzi wake kumi na wawili pembeni, akawaambia: “Tunapanda kwenda Yerusalema, na maneno yote yaliyoandikwa na manabii juu ya Mwana wa Mutu yatatimizwa.

32 Maana atatolewa katika mikono ya watu wa mataifa mengine. Watamuchekelea, watamutukana na kumutemea mate.

33 Watamupiga fimbo na kisha watamwua. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka!”

34 Wanafunzi wake hawakufahamu maana ya maneno hayo, kwa sababu yalikuwa yamefichwa kwao, nao hawakutambua kama Yesu alisema juu ya nini.


Yesu anamuponyesha kipofu
( Mat 20.29-34 ; Mk 10.46-52 )

35 Yesu alipokaribia muji Yeriko, mutu mumoja kipofu alikuwa akiikaa pembeni ya njia akiombaomba.

36 Aliposikia kundi la watu wakipita, akauliza juu ya mambo yanayopitika.

37 Wakamwambia kwamba ni Yesu wa Nazareti ndiye anayepita.

38 Basi akalalamika akisema: “Yesu Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!”

39 Watu waliotangulia wakamukaripia na kumunyamazisha, lakini alizidi kulalamika, akisema: “Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!”

40 Yesu akasimama, akaamuru wamulete kwake. Yule kipofu alipokaribia, Yesu akamwuliza:

41 “Unataka nikufanyie nini?” Akamujibu: “Bwana, ninataka nipate kuona.”

42 Yesu akamwambia: “Upate kuona! Imani yako imekuponyesha.”

43 Na pale pale akapata kuona, na kumufuata Yesu akishukuru Mungu. Na watu wote walipoona jambo hili wakamusifu Mungu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan