Luka 14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Yesu anaponyesha mugonjwa 1 Siku moja ya Sabato, Yesu aliingia katika nyumba ya mumoja wa wakubwa wa Wafarisayo kwa kula chakula. Mule watu wakabaki wakimuchunguza. 2 Na mbele ya Yesu kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa na ugonjwa wa kuvimba tumbo. 3 Basi Yesu akawauliza walimu wa Sheria na Wafarisayo: “Sheria inaruhusu au inakataza kuponyesha mutu kwa siku ya Sabato?” 4 Lakini wao wakanyamaza. Halafu Yesu akamushika mugonjwa, akamuponyesha na kumuruhusu kwenda. 5 Kisha akawaambia wale watu: “Ni nani kati yenu mutoto wake au ngombe wake akitumbukia ndani ya kisima, atakayekosa mara moja kumwondosha mule hata ikiwa ni siku ya Sabato?” 6 Nao hawakuweza kumujibu neno. 7 Yesu alipoona namna wale walioalikwa walivyojichagulia viti vya heshima, akawaambia mufano huu: 8 “Wakati mutu anapokualika kwa karamu ya ndoa, usiikae kwenye viti vya mbele. Labda kati ya waalikwa kuna mutu mwenye heshima kukupita. 9 Naye anapokuja, yule aliyewaalika ninyi wawili, ataweza kuja kukuambia: ‘Umwachie mutu huyu kiti.’ Halafu utapatwa na haya kwenda kuikaa kwenye viti vya nyuma. 10 Lakini wakati unapoalikwa, kwenda kuikaa kwenye viti vya nyuma, kusudi wakati yule aliyekualika atakapokuja, akuambie: ‘Rafiki, jongea huku mbele zaidi.’ Na halafu utaheshimiwa mbele ya wote unaoikaa pamoja nao kwa kula. 11 Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.” 12 Kisha Yesu akamwambia yule aliyemwalika: “Wakati unapofanya karamu ya muchana au ya magaribi, usiwaalike warafiki zako, wala wandugu zako, wala watu wa jamaa yako, wala jirani zako wanaokuwa watajiri, kusudi nao vilevile wasikualike, nawe usikuwe kama umelipwa. 13 Lakini wakati unapofanya karamu, uwaalike wamasikini, vilema, viwete na vipofu. 14 Hivi utabarikiwa, kwa maana watu hawa hawana cha kukulipa. Utalipwa hayo yote wakati wenye haki watakapofufuka.” Mufano wa karamu kubwa ( Mat 22.1-10 ) 15 Mutu mumoja kati ya wale waliokuwa wakiikaa kula pamoja na Yesu aliposikia maneno hayo, akamwambia: “Heri mutu atakayeshiriki kwa kula karamu katika Ufalme wa Mungu!” 16 Halafu Yesu akawaambia mufano huu: “Mutu mumoja alifanya karamu kubwa, na kualika watu wengi. 17 Saa ya karamu ilipotimia akamutuma mutumishi wake kwenda kuwaambia walioalikwa kwamba wafike kwa maana vitu vyote viko tayari. 18 Lakini wao wote moja kwa moja wakaanza kutoa sababu zao za kutokufika. Wa kwanza akamwambia yule mutumishi: ‘Nimenunua shamba, nami ninapaswa kwenda kuliangalia. Tafazali, unisamehe.’ 19 Mwingine akamwambia: ‘Nimenunua ngombe kwa ajili ya kazi ya kulima, nami ninakwenda kuwapima. Tafazali, unisamehe.’ 20 Na mwingine akamwambia: ‘Mimi ninatoka kuoa siku hizi, na kwa sababu hii siwezi kuja.’ 21 Basi yule mutumishi akarudia na kumwelezea bwana wake maneno hayo yote. Halafu bwana wa nyumba akakasirika, na kumwambia: ‘Kwenda upesi katika nafasi za mukutano na katika barabara za muji, uwalete wamasikini, vilema, vipofu na viwete na kuwaingiza humu.’ 22 Kisha, yule mutumishi akarudia na kusema: ‘Bwana, nimetimiza sawa ulivyoniamuru, lakini kungali nafasi.’ 23 Halafu bwana wake akamwambia: ‘Kwenda katika njia kwenye vijiji na pembeni ya mashamba, uwalazimishe watu wafike kuingia, kusudi nyumba yangu ipate kujaa. 24 Kwa maana ninawaambia kwamba kati ya wale niliokuwa nimewaalika, hakuna hata mumoja wao atakayeonja vyakula vya karamu yangu.’ ” Maana ya kumufuata Yesu ( Mat 10.37-38 ) 25 Siku moja makundi mengi ya watu walikuwa wakimufuata Yesu nyuma. Yeye akageuka na kuwaambia: 26 “Mutu anayenifuata, atakuwa kweli mwanafunzi wangu kama akinipendelea mimi kuliko baba na mama yake, muke na watoto wake, wakaka na wadada zake. Na zaidi ya hii hapaswi kujipendelea yeye mwenyewe vilevile. 27 Mutu yeyote asiyejitolea kwa kubeba musalaba wake na kunifuata, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 28 Ni nani kati yenu anayetaka kujenga munara, atakayekosa kwanza kuikaa na kuhesabu mali yote atakayoitumia kwa kujenga kusudi ajue kama yuko na mali inayotosha kwa kumaliza? 29 Kwa maana akiweka musingi, na nyuma anashindwa kumaliza kujenga munara ule, wote wanaoona jambo lile wataanza kumuzarau, 30 wakisema: ‘Mutu huyu alianza kujenga, lakini hakuweza kumaliza!’ 31 Au ni mufalme gani anayetaka kwenda kupigana vita na mufalme mwingine, atakayekosa kwanza kuikaa na kujiuliza kama kwa nguvu za waaskari wake elfu kumi ataweza kumushinda adui yake anayekuja na waaskari elfu makumi mbili? 32 Yeye akiona kwamba hataweza, atamutumia yule mufalme mwingine ujumbe kwa kuomba mapatano ya amani, huyo mwingine anapokuwa angali mbali. 33 Ni vile inavyokuwa, hakuna mumoja wenu atakayeweza kuwa mwanafunzi wangu kama asipoacha vyote anavyokuwa navyo.” Chumvi ( Mat 5.13 ; Mk 9.50 ) 34 “Chumvi ni kitu kizuri. Lakini chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini kusudi ipate tena kukolea? 35 Haifai tena kitu wala kwa udongo wala kwa mboleo, lakini watu wanaitupa tu. Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo