Luka 13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Katika siku zile watu wamoja wakakuja kumwelezea Yesu habari juu ya wale watu wa Galilaya waliouawa na liwali Pilato walipokuwa wakichinja nyama za kutolea Mungu sadaka. 2 Yesu akawauliza: “Munazani kwamba Wagalilaya hawa waliuawa vile kwa sababu wao walikuwa wenye zambi kuliko Wagalilaya wengine wote? 3 Hakika si vile, lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao. 4 Vilevile munazani kwamba wale watu kumi na wanane waliokufa munara ulipowaangukia kule Siloamu, walikuwa wakosaji kuliko wakaaji wengine wote wa Yerusalema? 5 Hakika si vile: lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao.” Mufano wa muti usiozaa matunda 6 Kisha Yesu akawaambia mufano huu: “Mutu mumoja alikuwa na muti wa tini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu. Alikuja kutafuta matunda juu yake, lakini hakupata kitu. 7 Basi akamwambia mutunzaji wa hili shamba: ‘Sasa ni muda wa miaka mitatu ninakuja kutafuta matunda juu ya muti huu wa tini nami sipati kitu. Uukate! Muti huu unaharibu udongo bure.’ 8 Lakini yule mutunzaji wa shamba akajibu: ‘Bwana, uuache tena mwaka huu; nitalima pembenipembeni yake na kuutilia mboleo. 9 Hivi utaweza labda kutoa matunda mwaka kesho! Kama si vile, basi utaukata!’ ” Yesu anaponyesha mwanamuke siku ya Sabato 10 Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa akifundisha katika nyumba ya kuabudia. 11 Na mule ndani mulikuwa mwanamuke mumoja mugonjwa, aliyeshikwa na pepo kwa muda wa miaka kumi na minane. Mugongo wake ulikuwa umekunjama na hakuweza kuinuka hata kidogo. 12 Yesu alipomwona yule mwanamuke, akamwita, akamwambia: “Ewe mama, ugonjwa wako umepona.” 13 Halafu akaweka mikono juu yake kwa kumuponyesha. Na mara moja akainuka tena, na kumutukuza Mungu. 14 Lakini mukubwa wa nyumba ya kuabudia alichukizwa kwa sababu Yesu aliponyesha mutu kwa siku ya Sabato. Kwa hiyo akawaambia watu waliokusanyika pale: “Kuna siku sita za kazi. Basi mufike kwa kuponyeshwa katika siku zile, hapana kwa siku ya Sabato!” 15 Lakini Bwana akamujibu: “Ninyi wanafiki! Kuna mutu mumoja kati yenu anayekosa kumufungua ngombe au punda wake toka katika upango kwa siku ya Sabato kwa kumupeleka kunywa maji? 16 Sasa, mwanamuke huyu anayekuwa wa uzao wa Abrahamu, ambaye alifungwa na Shetani kwa muda wa miaka kumi na minane, haikumupasa afunguliwe katika kifungo hiki ingawa ni siku ya Sabato?” 17 Yesu aliposema vile, wapinzani wake wote wakafezeheka, lakini kundi lote la watu wote walifurahia matendo yote ya ajabu aliyoyatenda. Mufano wa mbegu ndogo sana ya haradali ( Mat 13.31-32 ; Mk 4.30-32 ) 18 Yesu akasema tena: “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaulinganisha na nini? 19 Unafanana na mbegu ya haradali mutu mumoja aliyotwaa na kuipanda katika shamba lake. Ikaota na kuwa muti mukubwa, nao ndege wakakuja kujenga chicha zao katikati ya matawi yake.” Mufano wa chachu ( Mat 13.33 ) 20 Yesu akasema tena: “Nitafananisha Ufalme wa Mungu na nini? 21 Unafanana na chachu mwanamuke mumoja aliyoitwaa na kuichanga na vipimo vitatu vya unga kwa kuponda mikate, hata yote ikapata kuvimba.” Mulango mwembamba ( Mat 7.13-14 , 21-23 ) 22 Yesu alipokuwa katika safari kwenda Yerusalema, alipita katika miji na vijiji akifundisha. 23 Mutu mumoja akamwuliza: “Bwana, ni watu wachache tu ndio watakaookolewa?” Halafu Yesu akawaambia: 24 “Mufanye nguvu muingie kwa kupitia mulango unaokuwa mwembamba; maana ninawaambia ninyi hakika: watu wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza. 25 “Mwenye nyumba atakapokwisha kusimama na kufunga mulango, ninyi mutabaki inje na kuanza kupiga hodi na kusema: ‘Bwana, utufungulie.’ Naye atawajibu: ‘Sijui munatokea wapi.’ 26 Halafu mutaanza kumwambia: ‘Sisi tulikula na kunywa pamoja nawe, na wewe ulifundisha katika barabara za muji wetu.’ 27 Lakini atawaambia tena: ‘Sijui munatokea wapi. Mutoke karibu nami, ninyi wote watenda maovu!’ 28 Na kule mutalia na kusaga meno, mutakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika Ufalme wa Mungu. Lakini ninyi mutakuwa mumetupwa inje! 29 Watu watakuja toka mashariki na magaribi, kaskazini na kusini, nao wataikaa kula chakula katika Ufalme wa Mungu. 30 Wanaokuwa wa mwisho, watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.” Yesu anaulilia Yerusalema ( Mat 23.37-39 ) 31 Kwa saa zile Wafarisayo wamoja walimwendea Yesu na kumwambia: “Ondoka hapa uende fasi ingine, maana mufalme Herode anataka kukuua.” 32 Yesu akawajibu: “Mwende kumwambia yule mbweha: ‘Leo na kesho nitafukuza pepo na kuponyesha wagonjwa, na kesho kutwa nitamaliza kazi yangu.’ 33 Lakini ninapaswa kuendelea na safari yangu leo, kesho na kesho kutwa, kwa sababu haipaswi nabii auawe inje ya Yerusalema. 34 “Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka! 35 Makao yenu yataachwa ukiwa. Lakini ninawaambia: tangia sasa hamutaniona tena mpaka mutakaposema: ‘Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana.’ ” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo