Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Kutoka 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu anamwita Musa

1 Siku moja, Musa alikuwa anachunga kundi la kondoo la baba mukwe wake Yetro, kuhani wa Midiani. Musa akapeleka kundi lile upande wa magaribi wa jangwa, akafika kwenye mulima Horebu, mulima wa Mungu.

2 Basi, malaika wa Yawe akamutokea katika mwali wa moto katikati ya kichaka. Musa akaangalia, akashangaa kuona kichaka kinawaka moto na wala hakiungui.

3 Basi, akajisemesha: “Sasa nitazunguka nipate kuona jambo hili la ajabu, kichaka kuwaka moto na kisiungue!”

4 Yawe alipoona kwamba Musa amegeuka kwa kuangalia kichaka, akamwita pale kutoka kichaka: “Musa! Musa!” Musa akaitika: “Niko hapa. Ninasikiliza!”

5 Yawe akamwambia: “Usikuje karibu! Vua viatu vyako kwa sababu pahali unaposimama ni pahali patakatifu.”

6 Kisha Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Musa akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumwangalia Mungu.

7 Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,

8 na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.

9 Hakika, kilio cha Waisraeli kimenifikia; nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.

10 Sasa, nitakutuma kwa mufalme wa Misri kusudi uwatoe watu wangu, watu wale wa Israeli, kutoka katika inchi ya Misri.”

11 Lakini Musa akamwambia Mungu: “Mimi ni nani hata nimwendee mufalme wa Misri na kuwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri?”

12 Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”

13 Halafu, Musa akamwambia Mungu: “Sasa, nikiwaendea Waisraeli na kuwaambia: ‘Mungu wa babu zenu amenituma kwenu’, nao wakiniuliza: ‘Jina lake ni nani?’, nitawaambia nini?”

14 Mungu akamujibu: “Mimi Ndimi Ninayekuwa. Uwaambie watu wa Israeli kwamba: Yule anayeitwa Ndimi Ninayekuwa amekutuma kwao.

15 Uwaambie Waisraeli kwamba: Yawe, Mungu wa babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutuma kwao. Hili ndilo jina langu milele, na hivi ndivyo nitakavyokumbukwa katika vizazi vyote.

16 Kwenda uwakusanye wazee wa Israeli na kuwaambia kwamba: Yawe, Mungu wa babu wao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutokea na kusema: ‘Nimewachunguza ninyi na kuyaona mambo munayotendewa katika inchi ya Misri!

17 Ninaahidi kwamba nitawatoa katika mateso yenu kule Misri na kuwapeleka katika inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. Nitawapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali.’

18 “Wao watakusikiliza, nawe pamoja na wazee wa Waisraeli mutamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: ‘Yawe, Mungu wa Waebrania, ametutokea. Sasa, uturuhusu tuende safari ya mwendo wa siku tatu katika jangwa, tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka.’

19 Ninajua kwamba mufalme wa Misri hatawaacha muende asipolazimishwa kwa mukono wenye nguvu.

20 Kwa hiyo nitaunyoosha mukono wangu na kupiga inchi ya Misri kwa maajabu ambayo nitayafanya kule. Kisha mufalme atawaacha muondoke.

21 “Tena nitafanya Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Wamisri na mutakapoondoka Misri, hamutatoka mikono mitupu.

22 Kila mwanamuke Mwebrania atamwomba jirani yake Mumisri, au mugeni wake anayekuwa katika nyumba yake, amupe vyombo vya feza na zahabu pamoja na nguo. Hivyo mutawavalisha watoto wenu wanaume na wanawake. Ndivyo mutakavyowanyanganya Wamisri mali yao.”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan