Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Teka haraka, nyanganya upesi

1 Yawe aliniambia hivi: Twaa ubao mukubwa, uandike juu yake maneno yanayosomeka waziwazi: “Teka haraka. Nyanganya Upesi.”

2 Basi, nikajipatia washuhuda wawili waaminifu ambao wangenishuhudia: Kuhani Uria na Zekaria mwana wa Yeberekia.

3 Nikalala na muke wangu ambaye vilevile ni nabii, akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Yawe akaniambia: Umupe mutoto huyo jina “Teka-haraka-nyanganya-upesi.”

4 Maana mbele mutoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka neno “Baba” au “Mama”, utajiri wa muji wa Damasiki na vitu walivyonyanganya kule Samaria vitapelekwa kwa mufalme wa Asuria.


Mufalme wa Asuria anakuja

5 Yawe alisema nami tena, akaniambia:

6 Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia,

7 basi, Bwana wao atawaletea mafuriko makubwa ya maji ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria na nguvu zake zote; yatafurika na kupita kingo zake.

8 Utaingia ndani ya inchi ya Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka kwenye shingo. Utaenea juu ya inchi yako yote, ee Emanueli!


Mipango ya bure ya watu

9 Muungane, enyi watu wa mataifa, na kufezeheshwa! Musikilize, enyi inchi za mbali katika dunia! Mujiweke tayari na kufezeheshwa. Mujiweke tayari na kufezeheshwa.

10 Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.


Maonyo kwa nabii

11 Yawe alinionya kwa nguvu nisifuate njia za watu hawa, akaniambia:

12 Musijiunge nao katika mashauri yao mabaya, wala musiogope yale wanayoyaogopa wala kuwa na hofu.

13 Munitambue mimi peke yangu, Yawe wa majeshi, kuwa mutakatifu. Muniogope na kuniabudu mimi peke yangu.

14 Mimi nitakuwa kimbilio. Nitakuwa vilevile kama jiwe la kujikwaa, jiwe kubwa la kuziangusha falme za Israeli na Yuda. Nitakuwa mutego wa kuwatega na kuwanasa wakaaji wa Yerusalema.

15 Watu wengi watajikwaa, wataanguka na kupondekana; watanaswa katika mutego huo na kukamatwa mateka.


Maonyo juu ya kushauriana na mizimu

16 Nitalinda agizo hilo na kuchunga mafundisho hayo kati ya wafuasi wangu.

17 Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.

18 Mimi pamoja na watoto Yawe alionipa ni kitambulisho na mufano katika Israeli kwa jina la Yawe wa majeshi anayekaa kwenye mulima Sayuni.

19 Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.

20 Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.


Taabu

21 Watu watatangatanga katika inchi, wenye kufazaika sana na wenye njaa. Na wakiwa na njaa, watakasirika na kumulaani mufalme wao vilevile na Mungu wao. Wataangalia juu mbinguni

22 na kuiangalia dunia, lakini wataona tu taabu, giza na mateso makubwa. Hakuna atakayeepuka giza hilo kubwa.


Mutoto amezaliwa kwetu

23 Lakini inchi ile iliyokuwa imepatwa na huzuni haitabaki siku zote katika giza hilo kubwa. Hapo zamani Mungu alizifezehesha inchi za Zebuluni na Nafutali, lakini siku zinazokuja atafanya kuwa na utukufu kandokando ya bahari, inchi inayokuwa ngambo ya Yordani, na hata Galilaya ambamo watu wa mataifa wanaishi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan