Isaya 6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu anamwita Isaya kuwa nabii 1 Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote, 2 na juu yake kulikuwa kumeikaa wamalaika. Kila mumoja alikuwa na mabawa sita: mawili kwa kufunika uso, mawili kwa kufunika mwili na mawili ya kuruka. 3 Walilalamikiana mumoja kwa mwengine hivi: Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yawe wa majeshi! Dunia yote imejaa utukufu wake. 4 Sauti yao iliitikisa misingi ya milango ya hekalu, nalo likajaa moshi. 5 Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi. 6 Basi, mumoja wa hao wamalaika akaruka na kunifikia, akiwa ameshika katika mukono koleo lililokuwa na kaa la moto alilolitwaa kwenye mazabahu. 7 Naye akinigusa nalo kwenye mudomo, akasema: Kaa hili limekugusa kwenye mudomo; umeondolewa kosa lako, umesamehewa zambi yako. 8 Kisha nikamusikia Yawe akisema: Nimutume nani? Ni nani atakayekuwa mujumbe wetu? Nami nikajibu: Niko hapa! Unitume mimi. 9 Naye akaniambia: Kwenda kuwaambia watu hawa hivi: Mutasikiliza sana, lakini hamutaelewa; mutaangalia sana, lakini hamutaona. 10 Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona. 11 Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa. 12 Nami Yawe nitawapeleka watu mbali, na kuifanya inchi yote kuwa matongo. 13 Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo