Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 57 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maonyo juu ya ibada za sanamu

1 Mutu wa haki akikufa, hakuna mutu anayejali; mutu mwema akihamishwa toka dunia, hakuna mutu anayefikiri na kusema: Mutu huyo mwema amehamishwa kusudi asipatwe na hasara,

2 kusudi apate kuingia kwenye amani. Watu wenye mwenendo sawa, watakuwa na amani na kupumzika.

3 Lakini Yawe anasema: Mukuje hapa ninyi wana wa wake wachawi; ninyi wazao wa wachawi, wazinzi na makahaba.

4 Ni nani munayemuchekelea? Munamuzomea nani na kumutoshea ulimi inje? Ninyi wenyewe ni waasi tangu mwanzo, ninyi ni kizazi kidanganyifu.

5 Ninyi munawaka tamaa kwenye miti ya mialo, na chini ya kila muti wenye kuwa na majani mabichi. Munawachinja watoto wenu na kuwatambikia katika mabonde na ndani ya nyufa za mawe.

6 Munachagua mawe laini katika mabonde, na kuyafanya kuwa mungu wenu. Munayamwangia sadaka ya kinywaji na kuyapelekea sadaka ya unga! Mimi nitatulizwa kwa vitu hivyo?

7 Mumeweka vitanda vyenu juu ya milima mirefu, na kwenda kule kwa kutambikia.

8 Nyuma ya milango na miimo mumetundika sanamu yenu. Ninyi munaniacha mimi. Mumevua nguo zenu na kupanda juu ya vitanda vyenu vipana. Mumelipa wapenzi wenu ambao munataka kulala nao. Halafu munatimiza tamaa zenu mbaya.

9 Munajipakaa marasi na mafuta kwa wingi kisha munakwenda kumwabudu Moleki. Munawatuma wajumbe wenu huko na huko, kujitafutia miungu ya kuabudu; hata kuzimu walifika.

10 Mulichoka na safari zenu ndefu, hata hivyo hamukukata tamaa; mulijipatia nguvu mupya, ndiyo maana hamukuzimia.

11 Mulimwogopa na kutishwa na nani hata mukasema uongo, mukaacha kunikumbuka mimi na kuacha kabisa kufikiri juu yangu? Mimi sikuwaambia kitu kwa muda murefu; ndiyo maana labda mukaacha kuniheshimu!

12 Munafikiri kwamba munafanya sawa, lakini nitayafichua matendo yenu, nayo miungu yenu haitawafalia kitu.

13 Mutakapolia kwa kuomba musaada, basi ile lundo ya sanamu zenu iwaokoe! Upepo utavipeperushia mbali; pumzi itavitupilia mbali. Lakini watakaotafuta kimbilio kwangu, watarizi inchi, mulima wangu mutakatifu utakuwa mali yao.


Huruma ya Mungu

14 Yawe anasema hivi: Mujenge! Mujenge! Mutayarishe njia! Muondoe vikwazo vyote katika njia ya watu wangu!

15 Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.

16 Maana sitaendelea kugombana wala kuwakasirikia siku zote, maana hao niliowaumba watazimia mbele yangu, nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uzima.

17 Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao; niliwaazibu, nikauficha uso wangu na kukasirika. Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.

18 Niliona mwenendo wao, lakini nitawaponyesha; nitawaongoza na kuwapa faraja, nitawatuliza hao wanaoomboleza.

19 Mimi nitawapa amani, amani kwa wanaokuwa mbali na wanaokuwa karibu! –Ni Yawe anayesema hivyo.– Mimi nitawaponyesha.

20 Lakini waovu ni kama bahari iliyochafuka, ambayo haiwezi kutulia; maji yake yanatupa matope na takataka.

21 Mungu wangu anasema hivi: Hakuna amani kwa watu waovu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan