Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 55 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mukuje hata kama hamuna feza

1 Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!

2 Mbona munatumia feza zenu kwa ajili ya kitu kisichokuwa chakula? Kwa nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha? Munisikilize mimi kwa uangalifu, nanyi mutakula vinavyokuwa vitamu, na kufurahia vinavyokuwa bora.

3 Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.

4 Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.

5 Sasa utayaita mataifa usiyoyajua, watu wa mataifa yasiyokutambua watakuja mbio kwenu, kwa sababu yangu mimi Yawe, Mungu wako; kwa sababu yangu mimi Mutakatifu wa Israeli niliyekufanya wewe upate utukufu.

6 Mumutafute Yawe wakati angali anaweza kupatikana, mumwombe musaada wakati angali karibu.

7 Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.

8 Maana mawazo yangu si kama mawazo yenu, wala njia zangu si kama njia zenu. –Ni ujumbe wa Yawe.–

9 Kama vile mbingu zinavyokuwa mbali na dunia, ndivyo njia zangu zinavyokuwa mbali na zenu, na mawazo yangu mbali na mawazo yenu.

10 Kama vile mvua na teluji inavyoshuka toka mbinguni, wala hairudi kule lakini inalowanisha udongo, kuuzalisha na kuchipukiza mimea, na kumupatia mupandaji mbegu na kuwapa watu chakula,

11 ni vilevile na neno langu mimi: halitanirudilia bila mafanikio, lakini litatimiza mapenzi yangu, litafikia shabaha nililoliwekea.

12 Mutatoka Babeli kwa furaha; mutaongozwa muende kwa amani. Milima na vilima mbele yenu vitapiga kelele na kuimba, na miti yote katika mashamba itawapigia mikono.

13 Pahali pa miiba kutaota miti ya shindano, na pahali pa michongoma kutaota misunobari. Hilo litakuwa jambo litakalowakumbusha watu juu ya mambo niliyotenda mimi Yawe, kitambulisho cha milele ambacho hakitafutwa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan