Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 54 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Upendo wa Mungu kwa Israeli

1 Yawe anasema hivi: Imba kwa shangwe, ewe unayekuwa tasa, wewe ambaye haujapata kuzaa! Piga kelele na kuimba kwa nguvu, wewe usiyepata kuzaa mutoto. Maana watoto wako wewe uliyeachwa watakuwa wengi kuliko wa yule anayekuwa na mume.

2 Panua nafasi katika hema yako, ongeza mapazia ya makao yako, usijali mali unayotumia. Urefushe kamba zako, na kuimarisha misumari yako;

3 maana utapanuka kila upande; wazao wako watarizi mataifa, miji iliyokuwa ukiwa itajaa watu.

4 Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.

5 Muumba wako atakuwa mume wako. Jina lake Yawe wa majeshi. Mukombozi wako ni Mutakatifu wa Israeli. Yeye anaitwa Mungu wa Ulimwengu Wote.

6 Yerusalema, Yawe amekuita tena. Ulikuwa kama vile muke aliyeachwa na kuhuzunika. Mungu wako anasema: Muke aliyeolewa akiwa kijana, anaweza kuachiliwa?

7 Nilikuacha kwa muda mufupi tu. Kwa huruma nyingi, nitakurudisha.

8 Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.

9 Nitafanya kama nilivyofanya wakati wa Noa. Wakati ule niliapa kwamba sitaifunika tena dunia kwa mafuriko ya maji. Basi sasa ninaapa kwamba sitakukasirikia tena wala sitakukaripia tena.

10 Milima inaweza kutoweka, vilima vinaweza kuondolewa, lakini rehema zangu kwako sitaziacha, agano langu la amani litaimarishwa. Ni Yawe anayekuhurumia anayesema hivyo.


Yerusalema mupya

11 Ewe Yerusalema, uliteseka, ulitaabishwa na kukosa wa kukufariji, lakini nitakujenga upya kwa mawe ya bei kali, misingi yako itakuwa ya mawe ya yakuti.

12 Minara yako nitaijenga kwa mawe ya akiki, milango yako kwa almasi, na ukuta wako kwa mawe ya bei kali.

13 Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.

14 Utaimarishwa katika haki, mbali na kaoneo, nawe hautaogopa kitu; mbali na hofu, maana haitakukaribia.

15 Mutu yeyote akikuja kukushambulia, hatakuwa ametumwa nami. Yeyote atakayekushambulia, ataangamia mbele yako.

16 Mimi ndiye niliyemwumba mufuaji wa vyuma, anayewasha moto wa makaa na kufua silaha. Ni mimi vilevile niliyemwumba mwangamizaji anayeangamiza.

17 Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan