Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu anaahidi kuisaidia Israeli

1 Mungu anasema hivi: Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize! Enyi mataifa mujitie moyo; mujitokeze na mujisemee, na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.

2 Ni nani aliyemwita shujaa toka mashariki, mutu ambaye anapata ushindi popote anapoenda? Mimi ninayaweka mataifa katika mikono yake, naye anawaponda wafalme chini ya miguu yake! Upanga wake unawafanya kuwa kama mavumbi, kwa upinde wake anawapeperusha kama maganda.

3 Yeye anawakimbiza na kupita kwa usalama; anaenda mbio bila kukanyaga chini.

4 Nani aliyefanya yote haya yatendeke? Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio? Mimi Yawe nipo tangu mwanzo, mimi nitakuwa hata milele.

5 Wakaaji wa mbali wameona mambo niliyotenda, wakaogopa; dunia yote inatetemeka kwa woga. Watu wote wamekusanyika, wakakuja.

6 Kila mumoja anamusaidia mwenzake akisema: Ujipe moyo!

7 Fundi anamusaidia mufuaji wa zahabu. Naye anayelainisha sanamu kwa hama, anamusaidia anayeiunga kwa misumari. Wote wanasema: Ni vizuri sana! Kisha wanaifunga kwa misumari isitikisike.

8 Sikiliza ewe Israeli, mutumishi wangu, wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua, wewe wa uzao wa Abrahamu, rafiki yangu;

9 wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia, niliyekuita toka mbali kwa mipaka ya dunia, wewe niliyekuambia: Wewe ni mutumishi wangu; mimi sikukutupilia, lakini nilikuchagua.

10 Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.

11 Kweli! Wote waliokukasirikia, watapata haya na kufezeheka. Wote wanaopingana nawe, watakuwa wa bure na kuangamia.

12 Utawatafuta hao wanaopingana nawe, hautawaona tena; wale wanaofanya vita nawe, watakuwa wameangamia.

13 Mimi ndiye Yawe, Mungu wako, ndiye ninayeshika mukono wako. Mimi ndiye ninayekuambia: Usiogope, nitakusaidia.

14 Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.

15 Nitawafanya mukuwe kama chombo cha kupepeta, chenye meno mapya na makali. Mutaipepeta milima na kuipondaponda; mutavisagasaga vilima kama maganda.

16 Mutaipepeta milima hiyo, nao upepo utaipeperushia mbali, zoruba itaitawanya huko na huko. Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe; mutaona utukufu kwa sababu yangu Mungu Mutakatifu wa Israeli.

17 Wamasikini na wakosefu wakitafuta maji lakini hawayapati, wakiwa wamekauka koo kwa kiu, mimi Yawe nitawajibu; mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.

18 Nitabubujisha mito kwenye milima mitupu, na chemichemi katika mabonde. Nitaigeuza jangwa kuwa ziwa la maji, na inchi kuwa chemichemi za maji.

19 Nitapanda miti kule katika jangwa: mierezi, mivinje, mijohoro, na mizeituni; nitaweka kule katika jangwa: miberoshi, shindano na misunobari.

20 Watu wataona jambo hilo, nao watatambua na kuelewa kwamba mimi Yawe nimetenda hayo, mimi Mutakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.

21 Yawe, Mufalme wa Yakobo, anasema: Enyi miungu ya mataifa, mulete maneno yenu, mukuje mujitetee!

22 Mujongee, mutuambie yatakayotukia. Mutuambie matukio ya kwanza yalikuwa gani, nasi tutafikiri juu yake. Au mututangazie jinsi yatakavyotimia, kusudi tujue yatakayokuja.

23 Mutuambie yatakayotokea nyuma, nasi tujue basi kama ninyi ni miungu. Mufanye kitu chochote, chema au kibaya, kusudi tushangae na kuogopa.

24 Hakika, ninyi si kitu kabisa. Hamuwezi kufanya kitu chochote. Anayechagua kuwaabudu ninyi ni chukizo.

25 Nimetokeza mutu toka kaskazini, naye amekuja; nimemuchagua mutu toka mashariki, naye atalitaja jina langu. Yeye atawakanyaga wafalme kama matope, kama vile mufinyanzi anavyoponda udongo wake.

26 Nani aliyetangaza haya tangu mwanzo, hata sisi tupate kuyatambua? Nani aliyetangulia kuyatangaza, kusudi sasa tuseme, alisema ukweli? Hakuna hata mumoja kati yenu aliyeyataja, wala hakuna aliyesikia maneno yenu.

27 Mimi ni yule wa kwanza. Nilitangaza kwa Sayuni, nikapeleka Yerusalema mujumbe wa habari njema.

28 Nimeangalia vizuri sana, lakini simwoni mutu yeyote; hakuna yeyote kati ya hao miungu anayeweza kushauri; nikiuliza, hakuna anayeweza kunijibu.

29 Miungu hiyo yote ni udanganyifu, haiwezi kufanya kitu chochote; sanamu zao ni upepo tu, hazina maana.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan