Isaya 38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mufalme Hezekia anagonjwa ( 2 Fal 20.1-11 ; 2 Sik 32.24-26 ) 1 Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: Yawe anasema hivi: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona. 2 Hezekia akageukia upande wa ukuta na kumwomba Yawe, 3 akisema: Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote, na kutenda mazuri mbele yako. Hezekia akalia kwa uchungu sana. 4 Kisha neno la Yawe lilimufikia Isaya kusema hivi: 5 Kwenda umwambie Hezekia kwamba: Mungu wa baba yako Daudi, anasema hivi: Nimesikia ombi lako na nimeyaona machozi yako. Basi, ninakuongezea miaka kumi na mitano ya kuishi. 6 Nitakuokoa wewe pamoja na muji huu toka katika mikono ya mufalme wa Asuria na kuulinda. 7 Isaya akamujibu: Hiki kitakuwa kitambulisho kwako kutoka kwa Yawe kwamba Yawe atafanya kama alivyoahidi. 8 Nitafanya kivuli kwenye daraja iliyojengwa na Ahazi, kirudi nyuma hatua kumi. Nacho kivuli kikarudi nyuma hatua kumi. 9 Kisha mufalme Hezekia alipopona, akatunga wimbo huu wa shukrani: 10 Nilisema: nikiwa mubichi kabisa, inanipasa niage dunia. Mimi nimepangiwa kwenda katika kuzimu siku zote zilizonibakilia. 11 Nilisema sitamwona tena Yawe, katika inchi ya wanaokuwa wazima; wala sitamwona mutu yeyote tena, kati ya wakaaji wa ulimwengu. 12 Makao yangu yameongolewa kwangu; kama hema la muchungaji; kama, mufumaji nimefika kwa mwisho wa kizingo cha maisha yangu; Mungu amekata nyuzi zinazokishika; hata mbele ya mwisho wa siku amenikomesha. 13 Usiku kucha nililia kwa kuomba musaada; kama simba, anavunjavunja mifupa yangu; muchana na usiku ananikomesha. 14 Ninalia kama mbaruwayi, ninaugua kama njiwa. Macho yangu yamefifia kwa kuangalia juu. Ee Bwana, ninateseka; ukuwe wewe usalama wangu! 15 Lakini niseme nini: yeye mwenyewe aliniambia, naye mwenyewe ametenda hayo. Usingizi wangu wote umenitoroka kwa sababu ya uchungu ndani ya moyo wangu. 16 Ee Bwana, sisi tunaishi kutokana na yote uliyotenda, kwa hayo yote mimi peke yangu vilevile ninaishi. Unirudishie afya, uniwezeshe kuishi. 17 Nilipata mateso makali kwa faida yangu; lakini umeyaokoa maisha yangu kutoka shimo la uharibifu, maana umezitupa zambi zangu nyuma yako. 18 Huko kuzimu mutu hawezi kukushukuru wewe; waliokufa hawawezi kukushukuru wewe. Wala wanaoshuka kule katika shimo hawawezi tena kutumainia uaminifu wako. 19 Wanaokuwa wazima ndio wanaokushukuru, kama na mimi ninavyofanya leo. Wababa wanajulisha watoto wao uaminifu wako. 20 Yawe ataniokoa. Nasi tutamusifu kwa nyimbo za vinubi siku zote za maisha yetu, katika nyumba ya Yawe. 21 Isaya alikuwa amesema: Mutwae mukate wa tini na kuuweka kwenye jipu lake, apate kupona. 22 Hezekia akauliza: Ni kitambulisho gani kitakachonijulisha kwamba mimi nitakwenda kwa nyumba ya Yawe? |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo