Isaya 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Fujo katika Yerusalema 1 Sasa, Bwana wetu Yawe wa majeshi ataondoa kutoka Yerusalema na inchi ya Yuda kila tegemeo: tegemeo lote la chakula na la kinywaji. 2 Ataondoa mashujaa na waaskari, waamuzi na manabii, waaguzi na wazee, 3 majemadari na wakubwa, washauri, wachawi wafundi na waganga wenye maarifa. 4 Mungu anasema: Nitaweka watoto kuwa wakubwa wao; watoto wachanga watawatawala. 5 Watu watatesana, kila mutu na mwenzake; vijana watawazarau wazee, na watu wa ovyo ovyo watawazarau wenye heshima. 6 Wakati huo mutu atamwambia ndugu yake wakiwa bado katika nyumba ya baba yao: Wewe uko na nguo; utakuwa mukubwa wetu. Kamata utawala juu ya mabomoko haya! 7 Lakini siku hiyo atasema: Mimi siwezi kuwa muponyaji. Ndani ya nyumba yangu hamuna chakula wala nguo. Musinifanye mimi kuwa mukubwa wenu. 8 Watu wa Yerusalema wamejikwaa, watu wa Yuda wameanguka, kwa sababu wanamupinga Yawe kwa maneno na matendo, wakizarau utukufu wake kati yao. 9 Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe. 10 Muwaambie watu wa haki jinsi wanavyokuwa na heri, maana watakula matunda ya matendo yao. 11 Lakini ole kwao watu waovu! Mambo yatawaendekea vibaya, maana yale waliyotenda yatawapata wao wenyewe. 12 Watu wangu watateswa na watoto; wanawake ndio watakaowatawala. Enyi watu wangu, wakubwa wenu wanawapotosha, wanavuruga njia munayopaswa kufuata. Yawe anawahukumu watu wake 13 Yawe yuko tayari kuanza mashitaki, anasimama kwa kuwahukumu watu wake. 14 Yawe anawashitaki wazee na wakubwa wa watu wake: Ninyi ndio mulioliharibu shamba la mizabibu; mali wamasikini walizonyanganywa ziko ndani ya nyumba zenu. 15 Muna haki gani kuwagandamiza watu wangu, na kuwatendea wamasikini vibaya? –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi. Maonyo kwa wanawake wa Yerusalema 16 Yawe anasema: Wanawake wa Sayuni wako na kiburi; wanatembea wakiinua kichwa juu, wakirembua macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, nao wanalilisha mikufu kwenye miguu yao. 17 Basi, mimi Yawe nitawaazibu; nitawanyoa nywele hao wanawake wa Sayuni, na kuwavua nguo za kufunika uchi wao. 18 Siku zinakuja ambapo Yawe atawanyanganya wanawake wa Yerusalema vitu vyote wanavyoringia: pete za miguu, vitana, mibano ya nywele, 19 pete za masikio, vikomo na vitambaa vya ushungi, 20 vitambaa vya kichwa, mikufu, mikaba iliyosokotwa, hirizi na mikufu ya kuleta bahati, 21 pete za vidole na pua, 22 nguo za sikukuu, kanzu, vitambaa vya kichwa na mifuko ya mikono, 23 nguo nzuri, shemizi nzuri, vioo na vitambaa mbalimbali. 24 Kwa pahali pa harufu ya marasi watatoa uvundo; kwa pahali pa mikaba mizuri watatumia kamba; kwa pahali pa nywele nzuri watakuwa na upaa; kwa pahali pa nguo nzuri watavaa magunia; uzuri wao wote utageuka kuwa haya. 25 Wanaume wenu wataangamia kwa upanga, watu wenu wenye nguvu watakufa katika vita. 26 Halafu watu watalia na kuomboleza kwenye milango ya muji; nao wataikaa ndani ya mavumbi katika ukiwa. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo