Isaya 24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Yawe ataiazibu dunia 1 Sasa Yawe anaiharibu dunia na kuifanya tupu. Atavuruga uso wa dunia na kuwatawanya wakaaji wake. 2 Kila mutu atapatwa na mambo yaleyale: mutu wa kawaida na kuhani; mutumwa na bwana wake; mujakazi na bibi wake; mwenye kununua na mwenye kuuzisha; mukopeshaji na mukopaji; mwenye kudai na mwenye kudaiwa. 3 Dunia itaharibiwa kabisa na kuangamizwa. Ni Yawe amesema hayo. 4 Dunia inakauka na kunyauka; ulimwengu unafazaika na kunyauka; mbingu zinafazaika pamoja na dunia. 5 Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele. 6 Kwa sababu hiyo laana inaiteketeza dunia, wakaaji wake wanateseka kwa ajili ya makosa yao. Wakaaji wa dunia wamepunguka, ni watu wachache tu waliobaki. 7 Mizabibu inanyauka, divai inakosekana. Wote waliokuwa wenye furaha sasa wanaugua kwa huzuni. 8 Mudundo wa ngoma umekoma, makelele na fujo vimetoweka; midundo ya vinubi imekomeshwa. 9 Hakuna tena kunywa divai na kuimba; kinywaji cha kulewesha kimekuwa uchungu kwa wakunywaji. 10 Muji wa fujo umejaa uharibifu; kila nyumba imefungwa kusudi mutu asiingie. 11 Kuna kilio katika barabara kwa kukosa divai; shangwe yote imekoma, furaha imetoweka katika dunia. 12 Muji ni mabomoko matupu; milango yake imevunjwavunjwa. 13 Kama vile zeituni chache tu juu ya mizeituni au tini chache tu juu ya muti wa tini, kisha kumaliza mavuno, ndivyo inavyokuwa katika inchi zote. 14 Watu wanalalamika, wanaimba kwa shangwe. Kutoka upande wa magaribi, wanatangaza ukubwa wa Yawe, 15 na wale wa upande wa mashariki wanamusifu. Watu wa mbali wanalisifu jina la Yawe, Mungu wa Israeli. 16 Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia, nyimbo za kumusifu Mungu anayekuwa mwenye haki. Lakini mimi ninasema: Ninakonda, kweli ninakonda. Ole kwangu mimi! Wadanganyifu wanaendelea kuwa wadanganyifu, udanganyifu wao unazidi kuwa mubaya zaidi. 17 Woga, mashimo na mitego, hivi ndivyo vinavyowangojea, enyi wakaaji wa dunia. 18 Mutu atakayekimbia sauti ya woga atatumbukia ndani ya shimo; na mutu atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika. 19 Dunia inavunjikavunjika, inapasuka na kutikiswatikiswa. 20 Inapepesuka kama mulevi, inayumbayumba kama kibanda. Imelemewa na muzigo wa zambi zake nayo itaanguka wala haitasimama tena. 21 Siku ile Yawe ataliazibu jeshi la anga vilevile na wafalme wa dunia. 22 Wote watakusanywa kama wafungwa katika shimo; watafungwa katika kifungo pamoja kwa miaka mingi, na kisha muda huo atawaazibu. 23 Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo