Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maono juu ya kuangamizwa kwa inchi ya Babeli

1 Ujumbe wa Mungu juu ya jangwa kando ya bahari. Kama upepo mukali unaovuma kutoka kusini, washambulizi wanakuja kutokea katika jangwa, kutoka katika inchi ya kutisha.

2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.

3 Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa. Maumivu mengi yamenishika, kama maumivu ya mama anayezaa. Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia; nimefazaika hata siwezi kuona.

4 Moyo unanidunda na woga umenishika. Nilitamani magaribi ifike, lakini ilipofika ikakuwa ya kutetemesha.

5 Chakula kimetayarishwa, mikeka zimetandikwa, sasa watu wanakula na kunywa. Kwa rafla, sauti inasikilika: Musimame enyi watawala! Muweke silaha tayari!

6 Bwana aliniambia: Kwenda uweke mulinzi; umwambie atangaze atakachoona.

7 Akiona kikundi, waaskari wapanda-farasi wawiliwawili, wapanda-ngamia na wapanda-punda, akuwe macho. Akuwe macho kabisa!

8 Kisha, huyo mulinzi akalalamika: Bwana, nimesimama juu ya munara wa ulinzi muchana kutwa, nimeshika zamu usiku kucha!

9 Angalia, wanakuja: waaskari wapanda-farasi wawiliwawili. Wanasema: Babeli umeanguka! Umeanguka! Sanamu zote za miungu yake zimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!

10 Ewe Israeli, watu wangu, enyi muliotwangwa na kupepetwa kama ngano. Sasa nimewaambia ninyi mambo niliyoyasikia kwa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli.


Ufunuo juu ya Edomu

11 Ujumbe wa Mungu juu ya Duma. Ninasikia mutu ananiita kutoka Seiri: Mulinzi, nini kipya leo usiku? Kuna kipya chochote leo usiku?

12 Nami mulinzi nikajibu: Asubui inakuja, vilevile usiku; ukitaka kuuliza, uliza tu; kwenda urudi tena.


Ufunuo juu ya inchi ya Arabia

13 Ujumbe wa Mungu juu ya Arabia. Enyi makundi ya wasafiri ya Dedani, mupige kambi leo usiku katika pori za Arabia.

14 Enyi wakaaji wa inchi ya Tema, muwape maji hao wenye kiu; muwapelekee chakula hao wakimbizi.

15 Maana wamekimbia mapanga, mapanga yaliyochomolewa, pinde zilizovutwa na ukali wa mapigano.

16 Maana Bwana aliniambia hivi: Katika muda wa mwaka mumoja, bila kuzidi wala kupunguka, utukufu wote wa Kedari utakwisha.

17 Wapigapinde wachache kati ya mashujaa wa watu wa Kedari ndio watakaobaki. Ni Yawe, Mungu wa Israeli, anayesema hivyo.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan