Isaya 20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Isaya anatembea bila nguo na viatu 1 Sargoni, mufalme wa Asuria, alimutuma jemadari wake mukubwa kushambulia muji wa Asidodi. Naye akaushambulia na kuuteka. 2 Miaka mitatu mbele ya pale, Yawe alimwambia Isaya mwana wa Amozi hivi: Kwenda uvue nguo ya gunia uliyokuwa umevaa katika kiuno, na viatu vyako. Isaya akafanya kama alivyoambiwa; akakuwa anatembea uchi na bila viatu. 3 Yawe akasema: Mutumishi wangu Isaya amekuwa akitembea uchi na bila viatu kwa muda wa miaka mitatu sasa, kama kitambulisho juu ya inchi za Misri na Kushi. 4 Basi, mufalme wa Asuria atawapeleka Wamisri na Wakushi kuwa wafungwa, wakubwa kama vile wadogo. Watapelekwa, nao watatembea uchi na bila viatu, matako wazi. Misri ipate haya! 5 Kisha wote waliotegemea Kushi na kujivunia Misri watajuta na kufazaika. 6 Wakati huo, wakaaji wa kandokando watasema: Muangalie yaliyowapata watu tuliowategemea na kuwakimbilia kuomba musaada watuokoe na mufalme wa Asuria! Na sasa, sisi tutaweza namna gani kupona? |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo