Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu ataazibu Asuria na Israeli

1 Ujumbe wa Mungu juu ya muji wa Damasiki. Damasiki utakoma kuwa muji; utakuwa lundo la mabomoko.

2 Miji inayokuwa chini yake imeachwa matongo milele. Itakuwa makao ya makundi ya nyama, wala hakuna mutu atakayewatisha.

3 Pango za Efuraimu zitatoweka, na utawala wa Damasiki utakwisha. Waaramu ambao watabaki wazima, hawatakuwa na utukufu zaidi kama wazao wa Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Watakaobaki katika Israeli

4 Siku hiyo, utukufu wa Yakobo utaporomoshwa, na unono wake utapotea.

5 Itakuwa kama wakati wa mavuno, wakati wamekwisha kuokota ngano, na kukusanya masuke katika mukono. Hakika, itakuwa kama bonde la Refaimu wakati wamekwisha kuvuna ngano.

6 Watabaki wachache kama vile kisha kuangusha matunda ya mizeituni: matunda mawili au matatu katika tawi la juu; mane, matano katika matawi yanayozaa sana. –Ni ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli.


Mwisho wa kuabudu sanamu

7 Siku hiyo, watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa huyo Mutakatifu wa Israeli.

8 Hawataelekea tena mazabahu ambazo ni kazi za vidole vyao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, ni kusema sanamu za mungu Ashera na mazabahu za kufukizia ubani.

9 Siku hiyo miji yao imara itaachwa matongo, kama miji ambayo Wahivi na Waamori waliihama walipokuwa wakiwakimbia wazao wa Israeli. Kila kitu kitakuwa uharibifu.

10 Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;

11 hata mukiifanya ikomae siku hiyohiyo muliyoipanda na kuifanya ichanue asubui hiyohiyo, mavuno yenu yatatoweka siku hiyo ya hasara na maumivu yasiyoweza kuponyeshwa.


Mataifa adui yanashindwa

12 Aha! Ngurumo ya watu wengi! Wananguruma kama bahari. Aha! Mulio wa watu wa mataifa! Yanatoa mulio kama wa maji mengi.

13 Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo; kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.

14 Wakati wa magaribi yanaleta hofu kubwa, lakini mbele ya asubui yametoweka! Ndilo litakalowapata wale wanaotukamata na kutunyanganya mali yetu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan