Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu ataiangamiza Moabu

1 Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Moabu. Muji wa Ari katika inchi ya Moabu umeangamizwa usiku; muji wa Kiri katika inchi ya Moabu umeangamizwa usiku.

2 Watu wa Diboni wamepanda katika hekalu pahali pa juu kwa kuomboleza, watu wa Moabu wanalia kwa ajili ya Nebo na Medeba; vichwa vyote vimenyolewa upaa, ndevu zao zote zimekatwa kabisa.

3 Wanapita katika njia wakivaa magunia. Kwenye paa za nyumba na viwanja vya muji watu wanalia na kukauka kwa machozi.

4 Watu wa Hesiboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikilika mpaka Yasa. Hata waaskari wa Moabu wanalia kwa sauti; mioyo yao inatetemeka.

5 Moyo wangu unaugua kwa ajili ya inchi ya Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Zoari, wanakimbia mpaka Egilati-Selisiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhiti wakilia, katika njia kwenda Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.

6 Kijito cha Nimurimu kimekauka; nyasi zimekauka, majani mabichi yamenyauka, hakuna chochote kinachoota hapo.

7 Wakimbizi wanavuka kijito cha Mierebi; wamebeba mali yao yote waliyopata, na kila kitu walichojiwekea kama akiba.

8 Kilio kimesikilika pote katika inchi ya Moabu, maombolezo yao yamefika Eglaimu, yamefika hata mpaka Beri-Elimu.

9 Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini Mungu ataongeza musiba wa Dimoni. Hao wachache watakaobaki wazima na kukimbia kutoka Moabu, watapelekewa simba wa kuwaua.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan