Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kurudi kutoka katika uhamisho

1 Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.

2 Watu wa mataifa watawasaidia Waisraeli kurudi katika inchi waliyopewa na Yawe. Na hapo watawatumikia Waisraeli kama watumwa. Wale waliowateka sasa watatekwa na Waisraeli, na watawatawala wale waliowatesa.


Mufalme wa Babeli kati ya wafu

3 Ewe Israeli, wakati Yawe atakapokufariji nyuma ya mateso, mahangaiko na utumwa uliofanyiwa,

4 utaimba wimbo huu wa kumuchekelea mufalme wa Babeli: Jinsi gani mutesaji alikomeshwa! Ukali wake umekomeshwa!

5 Yawe amelivunja gongo la waovu, ameivunja fimbo ya kifalme ya watawala,

6 ambayo walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma, na kuwatawala kwa kuwatesa bila huruma.

7 Sasa dunia yote ina utulivu na amani, kila mutu anaimba kwa furaha.

8 Miti ya shindano inafurahia kuanguka kwako, nayo mierezi ya Lebanoni pamoja inasema: Kwa vile sasa umeangushwa, hakuna mukata miti atakayekuja juu yetu!

9 Kuzimu nako kumechangamuka, kusudi ya kukupokea wakati utakapokuja. Kunaiamusha mizimu ikuje kukusalimia na wote waliokuwa wakubwa wa dunia; kunawasimamisha kutoka kwenye viti vyao vya kifalme wote waliokuwa wafalme wa mataifa.

10 Wote kwa pamoja watakuambia: Nawe sasa umekuwa zaifu kama sisi! Umekuwa kama sisi wenyewe!

11 Utukufu wako umeteremushwa kuzimu pamoja na muziki wa vinubi vyako. Chini mafunza ndio kitanda chako, na wadudu ndio blanketi yako!

12 Jinsi gani ulivyoporomoshwa toka mbinguni, wewe uliyekuwa nyota yenye kuangaza kwa mapambazuko. Jinsi gani ulivyoangushwa chini, wewe uliyeyashinda mataifa!

13 Wewe ulijisemesha ndani ya moyo wako: Nitapanda mpaka mbinguni; nitaweka kiti changu juu ya nyota za Mungu, nitaikaa juu ya mulima pahali miungu wanapokutana, huko mbali pande za kaskazini.

14 Nitapanda juu ya mawingu nitajifanya kuwa sawa na Mungu Mukubwa.

15 Lakini umeporomoshwa mpaka kuzimu; umeshushwa chini kabisa ndani ya shimo.

16 Watakaokuona watakutonolea macho, watakushangaa wakisema: Huyu ndiye aliyetetemesha dunia na kuzitikisa falme,

17 aliyegeuza dunia kuwa kama jangwa, akaangamiza miji yake, na kukataa kuwafungua wafungwa wake?

18 Wafalme wote wa mataifa wamezikwa kwa heshima kila mumoja ndani ya kaburi lake.

19 Lakini wewe umetupwa inje ya kaburi lako, kama mutoto wa kuchukiza aliyezaliwa mufu, kama maiti ambayo imekanyagwakanyagwa. Umelundikiwa maiti za waliouawa kwa upanga, waliotupwa ndani ya mashimo penye mawe.

20 Lakini wewe hautaunganishwa nao katika mazishi, maana uliiharibu inchi yako, uliwaua watu wako. Wazao wa waovu wasahauliwe kabisa!

21 Mujitayarishe kuwachinja watoto wake kwa sababu ya makosa ya baba zao, wasipate kuamuka na kukamata inchi, na kuijaza dunia yote miji yao.


Mungu ataangamiza Babeli

22 Nitaushambulia muji wa Babeli na kuuangamiza kabisa. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Nitaharibu kila kitu, muji wote, watoto na yeyote aliyebaki muzima. –Ni ujumbe wa Yawe.–

23 Nitaufanya kuwa makao ya nungunungu, na utakuwa tingitingi ya maji. Nami nitaufagilia mbali kwa ufagio wa maangamizi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Mwisho wa mateso yote

24 Yawe wa majeshi ameapa: Kama nilivyopanga, ndivyo itakavyokuwa; kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyokamilika.

25 Nitauvunja uwezo wa Waasuria katika inchi yangu; nitawakanyagakanyaga katika milima yangu. Nitawaondolea watu wangu nira yao ya unyanganyi, na muzigo wa mateso yao.

26 Huu ndio uamuzi wa Yawe juu ya dunia yote; hii ndiyo azabu atakayotoa juu ya mataifa yote.

27 Kama Yawe wa majeshi ameamua, nani atakayeweza kuvunja uamuzi wake? Kama anaunyoosha mukono wake kutoa azabu, ni nani atakayemupinga?

28 Mwaka mufalme Ahazi alipokufa, Mungu alitoa ujumbe huu:

29 Musishangilie, enyi Wafilistini wote, kwamba Asuria, fimbo iliyowapiga, imevunjika; maana, nyoka wa kawaida atazaa nyoka mwenye sumu, na nyoka mwenye sumu atazaa nyoka mukubwa mwenye kuruka.

30 Wazaliwa wa kwanza wa wazaifu watashiba, na wakosefu watakaa kwa usalama. Lakini chipukizi wenu nitawaua kwa njaa; na yeyote kati yenu atakayebaki nitamwua.

31 Ulie ewe mulango; ulalamike ewe muji; tetemeka kwa hofu, ewe inchi yote ya Filistia. Maana moshi wa waaskari unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika makundi yake.

32 Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo? Wataambiwa: Yawe ameijenga imara Sayuni, na wamasikini kati ya watu wake watakimbilia kule.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan