Isaya 11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Ufalme wa amani 1 Kutatokea chipukizi katika shina la Yese, tawi litachipuka toka mizizi yake. 2 Roho wa Yawe atakaa kwake, Roho wa hekima na maarifa, Roho wa shauri jema na nguvu, Roho wa akili na utii wa Mungu. 3 Furaha yake itakuwa kumutii Yawe. Hatatoa hukumu kulingana na yale anayoona, wala kuamua kufuatana na yale anayosikia. 4 Atawaamulia wamasikini kwa haki na kutetea haki za wakosefu katika inchi. Kwa neno lake dunia itaazibiwa, kwa pumzi yake waovu watauawa. 5 Haki itakuwa kama mukaba wa kujifunga, uaminifu utakuwa kama mukaba kwenye kiuno chake. 6 Imbwa wa pori ataishi pamoja na mwana-kondoo, chui atapumzika pamoja na mwana-mbuzi. Wana-ngombe na wana-simba watakula pamoja, na mutoto mudogo atawaongoza. 7 Ngombe na dubu watakula pamoja, watoto wao watapumzika pamoja; na simba atakula majani kama ngombe. 8 Mutoto muchanga atacheza kwenye shimo la nyoka, mutoto ataweza kutia mukono kwenye shimo la nyoka wa sumu. 9 Katika mulima mutakatifu wa Mungu hakutakuwa ubaya wala uharibifu. Maana kumujua Yawe kutaenea pote katika inchi, kama vile maji yanavyojaa katika bahari. Wanaokuwa katika uhamisho watarudia 10 Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka. 11 Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari. 12 Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia. 13 Wivu wa Efuraimu juu ya Yuda utakoma, hakutakuwa tena uadui kati ya Yuda na Efuraimu. 14 Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi, pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki. Watawashinda Waedomu na Wamoabu, nao Waamoni watawatii. 15 Yawe atakausha guba ya bahari ya Misri, kwa pumzi yake inayochoma atakausha muto Furati, nao utagawanyika katika vijito saba, watu wavuke humo miguu mikavu. 16 Tena, kutakuwa barabara kubwa toka Asuria kwa ajili ya watu wake waliobaki humo kama ilivyokuwa kwa Waisraeli wakati walipotoka katika inchi ya Misri. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo