Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Isaya 10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ole kwao wanaotunga sheria za uovu, watu wanaopitisha sheria za kugandamiza.

2 Wanakataa kusambisha wazaifu, wananyanganya watu wangu wamasikini haki yao. Wanateka wajane; wananyanganya wayatima mali yao.

3 Mutafanya nini siku ya azabu, siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali? Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada? Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?

4 Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Maonyo kwa mufalme wa Asuria

5 Ole kwake Asuria, yeye ni kama fimbo ya hasira yangu, yeye anayeshika kiboko cha hasira yangu!

6 Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.

7 Lakini Asuria hakuwazia hivyo, yeye alikuwa na nia ingine; alikusudia kuharibu kabisa, kuangamiza mataifa mengi sana.

8 Maana alisema: Si kweli majemadari wangu ni wafalme?

9 Si kweli kwamba muji wa Kalno niliutendea kama vile wa Karkemisi, muji wa Hamati kama muji wa Arpadi, Samaria kama Damasiki?

10 Nimepata kuunyoosha mukono wangu juu ya falme zenye sanamu za miungu kubwa kuliko sanamu za Yerusalema na Samaria.

11 Basi nitashindwa kuutendea Yerusalema na sanamu zake, kama nilivyoutendea Samaria na sanamu zake?

12 Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.

13 Maana mufalme wa Asuria alisema: Kwa nguvu zangu mwenyewe nimetenda hayo, na kwa hekima yangu, maana mimi ni mwerevu! Nimeondoa mipaka kati ya mataifa, nikanyanganya akiba zao; kama ngombe dume nimewaporomosha walioikaa juu ya viti vya kifalme.

14 Kama mutu anayenyoosha mukono kwenye chicha, ndivyo nilivyokamata mali ya mataifa; kama mutu anayeokota mayai yaliyoachwa ndani ya chicha, ndivyo nilivyoyaokota katika dunia yote. Watu wote walikuwa sawa ndege ambaye hapigi mabawa au kufungua midomo kwa kupiga kelele. Lakini Yawe anasema hivi:

15 Shoka litaweza kujisifu mbele ya yule anayelitumia? Musumeno unaweza kujivuna mbele ya mwenye kukata nao? Ni kama kwamba vile fimbo ingeweza kumwinua anayeishika, au gongo kumwinua mwenye kuitumia!

16 Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi, atawaletea waaskari wao wanene ugonjwa wa kuwakondesha, na utukufu wao utateketezwa kama kwa moto.

17 Mungu anayekuwa mwangaza wa Israeli atakuwa kama moto. Mutakatifu wa Israeli atakuwa ulimi wa moto ambao kwa siku moja utateketeza kila kitu, miiba yake na michongoma zake pamoja.

18 Pori yake yenye utukufu na mashamba yake mazuri, Yawe atayaangamiza yote; itakuwa kama mutu aliyemalizika na ugonjwa.

19 Miti itakayobaki katika pori yake itakuwa michache sana hata mutoto mudogo ataweza kuihesabu.


Wachache watarudi

20 Siku ile wazao wa Yakobo watakaobaki, ni kusema Waisraeli watakaopona hawatalitegemea tena taifa lililowaazibu, lakini watamutegemea kabisa Yawe, Mutakatifu wa Israeli.

21 Wazao wa Yakobo wachache watakaobaki watamurudilia Mungu Mukubwa.

22 Maana, hata kama sasa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaorudi. Maangamizi yamepangwa yafanyike, nayo yatafanyika kwa haki tu.

23 Kweli! Bwana, Yawe wa majeshi, atakamilisha kabisa katika inchi yote jambo aliloamua kutenda.


Yawe ataiazibu inchi ya Asuria

24 Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.

25 Maana bado kidogo, nayo hasira yangu itapita na kasirani yangu itawageukia Waasuria.

26 Yawe wa majeshi atainua fimbo yake kama vile alivyowapiga Wamidiani kwenye jiwe la Orebu. Atanyoosha fimbo yake juu ya bahari kama vile alivyowafanyia Wamisri.

27 Wakati huo, muzigo waliowabebesha atauondoa na nira waliyowatia kwenye shingo lenu itavunjwa. Adui amepanda kutoka Rimoni,


Adui anakaribia

28 amefika katika muji wa Ayati. Amepitia kule Migoroni, mizigo yake ameiacha katika muji wa Mikimasi.

29 Amekwisha pita kwenye kivuko. Usiku huu analala Geba. Watu wa Rama wanatetemeka kwa hofu, wakaaji wa Gibea, muji wa Sauli, wamekimbia.

30 Enyi watu wa Galimu, mupige kelele! Enyi watu wa Laisi, mutege sikio! Enyi wenyeji wa Anatoti, mujibu!

31 Watu wa Madimena wamekimbia, wakaaji wa Gebimu wanatafuta makimbilio.

32 Leo hii, adui atapiga kambi kule Noba, anainua mukono wake kwa mulima Sayuni, kilima cha Yerusalema.

33 Bwana, Yawe wa majeshi atakata matawi kwa ukali, miti mirefu itaangushwa chini, wanaokuwa juu watashushwa.

34 Atakata vichaka vya pori kwa shoka; Lebanoni na mierezi yake yenye utukufu itaanguka.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan