Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hosea 9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Hosea anatangaza azabu ya Israeli

1 Musifurahi enyi Waisraeli! Musishangilie kama watu wa mataifa mengine; maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu. Mumefurahia malipo ya uzinzi, kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.

2 Hawatapata chakula kutoka kiwanja cha kupepetea, hawatapata divai mupya kutoka kikamulio.

3 Hawatakaa katika inchi ya Yawe. Watu wa Efuraimu watarudi katika utumwa kule Misri. Watakula vyakula vichafu kule Asuria.

4 Hawatamutolea Yawe sadaka ya divai, wala hawatamufurahisha kwa sadaka zao. Chakula chao kitakuwa kama cha kilio, wote watakaokikula watajichafua. Kitakuwa chakula cha kuwashibisha tu, hakitafaa kuletwa katika nyumba kwa Yawe.

5 Mutafanya nini katika sikukuu ile iliyopangwa, au katika karamu ya Yawe?

6 Mutakapoyakimbia maangamizi ya inchi yenu, Misri itawakaribisha ninyi kwake, lakini makaburi yenu yanawangoja kule Memufisi. Michongoma itaota katika vyombo vyenu vya feza, miiba itajaa katika mahema yenu.

7 Siku za azabu zimetimia, siku za kulipiza kisasi zimefika; Waisraeli lazima wautambue wakati huo! Ninyi munasema: Nabii ni mupumbafu; anayeongozwa na roho ni mwenda-wazimu. Munasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mukubwa, kwa sababu ya chuki yenu kali juu yake.

8 Nabii ni mulinzi wa Waefuraimu kwa pahali pa Mungu; lakini, popote anapoenda anategewa mutego kama ndege. Hata katika nyumba ya Mungu wake anachukiwa.

9 Ninyi mumezama katika uovu, kama ilivyokuwa kule Gibea. Mungu atayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Zambi ya Israeli na matokeo yake

10 Yawe anasema: Nilipowakuta Waisraeli walikuwa kama zabibu katika jangwa. Nilipowaona babu zenu, walikuwa bora kama matunda ya tini za kwanza. Lakini walipofika kule Bali-Peori, wakajitolea kwa kuabudu chukizo Bali, wakakuwa chukizo kama kile walichokipenda.

11 Utukufu wa Efuraimu utatoweka kama ndege; watoto hawatazaliwa tena, hakutakuwa watoto wa kuzaliwa, wala hakutakuwa atakayepata mimba!

12 Hata kama wakilea watoto, sitamwacha hata mumoja wao muzima. Ole kwao, nitakapowaacha peke yao!

13 Zamani, niliona kwamba Efuraimu ilikuwa kama muti wa ngazi muchanga kwenye nafasi nzuri. Lakini sasa Efuraimu italazimishwa kuwapeleka watoto wake wauawe.

14 Uwaazibu watu hawa, ee Yawe! Lakini utawaazibu namna gani? Uwafanye wanawake wao kuwa tasa; uwafanye wakose maziwa ya kunyonyesha watoto wao!


Hukumu ya Yawe kwa Israeli

15 Yawe anasema hivi: Uovu wao wote ulianzia Gilgali; kule ndiko nilipoanza kuwachukia. Kwa sababu ya uovu wa matendo yao, nitawafukuza toka katika nyumba yangu. Sitawapenda tena. Wakubwa wao wote ni waasi.

16 Watu wa Efuraimu wamepigwa, wamekuwa kama muti wenye muzizi wenye kukauka, hawatazaa watoto wowote. Hata kama wakizaa watoto, nitawaua watoto wao wanaowapenda.

17 Kwa vile wamekataa kumusikiliza, Mungu wangu atawatupilia; wao watatangatanga kati ya mataifa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan