Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hosea 8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Makosa makubwa ya Israeli

1 Mupige baragumu! Adui anakuja kama tai kuishambulia nyumba ya Yawe, kwa sababu wamelivunja agano langu na kuiasi sheria yangu.

2 Waisraeli wananililia wakisema: Mungu wetu, sisi tunakujua.

3 Lakini Waisraeli wametupilia mambo mazuri. Kwa hiyo, sasa waadui watawafuatilia.

4 Walijiwekea wafalme bila ruhusa yangu, walijichagulia wakubwa ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya feza na zahabu, jambo ambalo litawaangamiza.

5 Enyi watu wa Samaria, ninaichukia sanamu yenu ya mwana-ngombe. Hasira yangu inawaka juu yenu. Mutaendelea kuwa na makosa mpaka wakati gani?

6 Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!

7 Wanapanda upepo, watavuna zoruba! Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba haitatoa ngano yoyote. Na hata kama ikizaa, mazao yake yatakuliwa na wageni.

8 Waisraeli wamemezwa, wanakuwa kati ya mataifa mengine, kama chombo kisichokuwa na faida yoyote.

9 Wamekwenda kuomba musaada Asuria. Efuraimu ni punda wa pori anayetangatanga peke yake; Efuraimu amejilipia wapenzi wake.

10 Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa, lakini mimi nitawakusanya. Na hapo watasikia uzito wa muzigo wa mufalme wa wakubwa.

11 Watu wa Efuraimu wamejijengea mazabahu nyingi, na mazabahu hizo zimewazidishia zambi.

12 Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi, wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.

13 Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.

14 Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan