Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hosea 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Watu wa Efuraimu wananizunguka kwa uongo, na Waisraeli kwa udanganyifu. Lakini watu wa Yuda wanaendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu Mutakatifu.

2 Watu wa Efuraimu wanachunga upepo, muchana kutwa wanafukuza upepo wa mashariki. Wanazidisha uongo na mateso, wanafanya mapatano na Asuria na kupeleka mafuta Misri.

3 Yawe ana mashitaki juu ya Yuda; atawaazibu wazao wa Yakobo kadiri ya makosa yao, na kuwalipa kadiri ya matendo yao.

4 Yakobo akiwa angali katika tumbo la mama yake, alimushika kaka yake kisigino. Na alipokuwa mutu muzima alishindana na Mungu.

5 Alipigana na malaika, akamushinda; alilia machozi na kuomba ahurumiwe. Kule Beteli, alikutana na Mungu, na kusemezana naye,

6 Yawe wa majeshi, Yawe, ndilo jina lake.

7 Lakini ninyi mumurudilie Mungu wenu. Mushikamane na wema na haki, mumutumainie Mungu wenu siku zote.

8 Efuraimu ni sawa na muchuuzi anayetumia vipimo vya udanganyifu, anayependa kudanganya watu.

9 Efuraimu amesema: Mimi ni tajiri! Mimi nimejitajirisha! Sikufanya mabaya kwa kupata hii faida.

10 Yawe anasema: Mimi ni Yawe, Mungu wako, tangia katika inchi ya Misri! Mimi nitakukalisha tena katika mahema, kama vile mulivyofanya wakati nilipokutana nanyi.

11 Mimi niliongea na manabii; ni mimi niliyewapa maono mengi, na kwa njia yao nilitangaza mupango wangu.

12 Watu wa Gileadi walikuwa waovu sana; hakuna tena kitu kinachokuwa chao. Kule Gilgali walitambikia ngombe dume. Hivyo, mazabahu zao zitakuwa malundo ya mawe yaliyowekwa kwa mafungu katika shamba.

13 Yakobo alikimbilia katika inchi ya Aramu. Akiwa huko alifanya kazi kusudi apate mwanamuke, akachunga kondoo kusudi apate mwanamuke.

14 Kwa njia ya nabii, Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri. Kwa njia ya nabii, Mungu aliwalinda.

15 Waefuraimu wamemuchukiza Yawe sana. Lakini Yawe atawalipiza makosa yao, atawaazibu kwa mambo maovu waliyotenda.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan