Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hosea 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hili ni neno ya Yawe lililomufikia Hosea mwana wa Beri katika siku za utawala wa Uzia, Yotamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi, mufalme wa Israeli.


Muke na watoto wa Hosea

2 Yawe alipoanza kusema na Waisraeli kwa njia ya Hosea, alimwambia hivi: Kwenda kuoa mwanamuke muzinzi, uzae naye watoto wa uzinzi, maana watu wa inchi hii wanafanya uzinzi mwingi kwa kuniacha mimi.

3 Basi, Hosea akaenda, akamwoa Gomeri, binti wa Dibulaimu. Gomeri akapata mimba, akamuzalia Hosea mutoto mwanaume.

4 Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Yezereheli”, maana kisha siku chache tu, nitaiazibu jamaa ya Yehu kwa mauaji aliyofanya katika bonde la Yezereheli. Hivi nitavunja ufalme katika taifa la Israeli.

5 Siku hiyo, nitazivunja nguvu za makundi ya waaskari wa Israeli kule katika bonde la Yezereheli.

6 Gomeri alipata mimba tena, akazaa mutoto mwanamuke. Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Asiyehurumiwa”, maana sitawahurumia tena Waisraeli wala sitawasamehe.

7 Lakini nitawahurumia watu wa Yuda na kuwaokoa. Mimi Yawe, Mungu wao, nitawaokoa, lakini si kwa nguvu za waaskari, au pinde, au panga, au farasi au waaskari wapanda-farasi.

8 Gomeri alipomwachisha yule binti wake Asiyehurumiwa kunyonya, alipata mimba tena, akazaa mutoto mwingine mwanaume.

9 Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Si wangu”, maana ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan