Hesabu 33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Safari kutoka Misri mpaka Moabu 1 Hivi ndivyo vituo ambavyo Waisraeli wakapiga kambi walipotoka Misri wakiwa katika makundi ya makabila yao chini ya uongozi wa Musa na Haruni. 2 Musa aliandika jina la kila pahali walipopiga kambi, kituo kwa kituo, kwa agizo la Yawe. 3 Waisraeli wakaondoka katika muji wa Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku moja nyuma ya Pasaka ya kwanza. Wakaondoka kwa uhodari mukubwa mbele ya Wamisri wote, 4 ambao walikuwa wanazika wazaliwa wao wa kwanza wanaume Yawe aliowaua; maana Yawe alikuwa ameiazibu hata miungu yao. 5 Basi, Waisraeli wakaondoka Ramesesi, wakapiga kambi yao huko Sukoti. 6 Kutoka Sukoti, wakapiga kambi yao huko Etamu, kwenye ukingo wa jangwa. 7 Kutoka Etamu, waligeuka na kurudi mpaka Pi-Hahiroti, upande wa mashariki wa Bali-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migidoli. 8 Wakaondoka Pi-Hahiroti, wakapita bahari Nyekundu mpaka jangwa la Etamu; wakasafiri katika jangwa mwendo wa siku tatu, wakapiga kambi yao Mara. 9 Kutoka Mara, wakasafiri mpaka Elimu; huko Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na mingazi makumi saba, wakapiga kambi yao pahali pale. 10 Wakasafiri kutoka Elimu, wakapiga kambi yao karibu na bahari ya Nyekundu. 11 Kutoka bahari Nyekundu wakapiga kambi yao katika jangwa la Sini. 12 Kutoka jangwa la Sini, wakapiga kambi yao Dofuka. 13 Kutoka Dofuka wakapiga kambi yao huko Alusi. 14 Kutoka Alusi wakapiga kambi yao huko Refidimu, ambapo hapakukuwa maji ya kunywa. 15 Wakaondoka Refidimu wakapiga kambi yao katika jangwa la Sinai. 16 Kutoka Sinai wakapiga kambi yao huko Kibroti-Hatawa. 17 Kutoka Kibroti-Hatawa, wakapiga kambi yao huko Haseroti. 18 Kutoka Haseroti, wakapiga kambi yao huko Ritima. 19 Kutoka Ritima, wakapiga kambi yao huko Rimoni-Perezi. 20 Kutoka Rimoni-Perezi, wakapiga kambi yao huko Libuna. 21 Kutoka Libuna wakapiga kambi yao Risa. 22 Waliondoka Risa, wakapiga kambi yao huko Kehelata. 23 Kutoka Kehelata, wakapiga kambi yao kwenye mulima Seferi. 24 Kutoka mulima Seferi wakapiga kambi yao huko Harada. 25 Kutoka Harada, wakapiga kambi yao huko Makeloti. 26 Kutoka Makeloti, wakapiga kambi yao huko Tahati. 27 Kutoka Tahati wakapiga kambi yao Tera. 28 Kutoka Tera wakapiga kambi yao Mitika. 29 Kutoka Mitika, wakapiga kambi yao Hasimona. 30 Kutoka Hasimona, wakapiga kambi yao Musaroti. 31 Kutoka Musaroti, wakapiga kambi yao Bene-Yaakani. 32 Kutoka Bene-Yaakani, wakapiga kambi yao Hori-Hagidigadi. 33 Kutoka Hori-Hagidigadi, wakapiga kambi yao Yotibata. 34 Kutoka Yotibata, wakapiga kambi yao Abarona. 35 Kutoka Abarona, wakapiga kambi yao Esioni-Geberi. 36 Waliondoka Esioni-Geberi, wakasafiri na kupiga kambi yao katika jangwa la Sini, ni kusema Kadesi. 37 Kutoka Kadesi, wakapiga kambi yao juu ya mulima Hori, kwenye mupaka wa inchi ya Edomu. 38 Kwa agizo la Yawe kuhani Haruni akapanda juu ya mulima Hori, na huko, akakufa katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa makumi ine tangu Waisraeli walipotoka katika inchi ya Misri. 39 Haruni alikuwa na umri wa miaka mia moja makumi mbili na mitatu alipokufa juu ya mulima Hori. 40 Mufalme wa Aradi, Mukanana, aliyekaa Negebu katika inchi ya Kanana akapata habari kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja. 41 Kutoka mulima Hori, Waisraeli wakapiga kambi yao Salmona. 42 Kutoka Salmona, wakapiga kambi yao Punoni. 43 Kutoka Punoni, wakapiga kambi yao Oboti. 44 Kutoka Oboti, wakapiga kambi yao Iye-Abarimu, katika eneo la Moabu. 45 Kutoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi yao Diboni-Gadi. 46 Kutoka Diboni-Gadi, wakasafiri na kupiga kambi yao Almoni-Diblataimu. 47 Kutoka Almoni-Diblataimu, wakasafiri na kupiga kambi yao katika milima ya Abarimu, karibu na mulima Nebo. 48 Kutoka milima ya Abarimu, wakasafiri na kupiga kambi yao katika mabonde ya Moabu ngambo ya muto Yordani karibu na Yeriko. 49 Wakapiga kambi hiyo karibu na muto Yordani kati ya Beti-Yesimoti na bonde la Abeli-Sitimu kwenye mabonde ya Moabu. 50 Katika mabonde ya Moabu, ngambo ya muto Yordani karibu na Yeriko, Yawe akamwambia Musa: 51 Uwaambie Waisraeli kwamba mutakapovuka muto Yordani na kuingia katika inchi ya Kanana, 52 muwafukuze wenyeji wote wa inchi hiyo mbele yenu. Mutaziharibu sanamu zao zote za mawe na za kuyeyushwa na kubomoa kila pahali pao pa ibada. 53 Mutatwaa inchi hiyo na kukaa mule kwa sababu nimewapa muirizi. 54 Mutagawanya inchi hiyo kwa kura kufuata jamaa zenu; eneo kubwa kwa kabila kubwa na eneo dogo kwa kabila dogo. 55 Lakini kama musipowafukuza wenyeji wa inchi hiyo kwanza, basi wale mutakaowaacha watakuwa kama vile sindano ndani ya macho yenu au miiba kila upande, na watawasumbua. 56 Nami nitawafanya ninyi kama vile nilivyokusudia kuwafanya wao. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo