Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hesabu 30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Basi, Musa akawaambia Waisraeli kila kitu kama vile Yawe alivyomwamuru.


Maagizo juu ya viapo

2 Kisha Musa akazungumuza na viongozi wa makabila ya Israeli, akawaambia: Hili ndilo neno lililoamriwa na Yawe:

3 Mutu akiahidi mbele ya Yawe au akifanya kiapo, anapaswa kutimiza ahadi yake. Anapaswa kushika yale yote aliyotamka kwa kinywa chake.

4 Binti ambaye angali anaishi katika nyumba ya baba yake akiahidi mbele ya Yawe na kufanya kiapo,

5 na baba yake akisikia ahadi hiyo naye hamupingi, yule binti atafungwa na kila kiapo na ahadi aliyofanya.

6 Lakini kama baba yake akisikia juu ya kiapo hicho, akimupinga, basi kiapo chake au ahadi yake havitamufunga. Yawe atamusamehe kwa sababu baba yake amelipinga jambo hilo.

7 Ikiwa binti ataolewa kisha kufanya kiapo au kuahidi bila kufikiri vizuri kwanza,

8 halafu mume wake akisikia jambo hilo naye hamupingi, muke wake atafungwa na kila kiapo au ahadi aliyofanya.

9 Lakini kama mume wake akisikia jambo hilo, akimupinga, basi huyo mume wake atavunja kiapo cha muke wake na maneno yale aliyosema bila kufikiri; naye Yawe atamusamehe.

10 Lakini kiapo au ahadi yoyote mujane aliyoweka au mwanamuke aliyeachana na mume wake ambayo kwa njia yake amejifunga, inapaswa kumufunga.

11 Mwanamuke aliyeolewa akifanya ahadi au kiapo akiwa katika nyumba ya mume wake,

12 kisha mume wake akisikia jambo hilo naye hamupingi, wala kumwambia kitu, basi, viapo vyake vyote vitamufunga; vilevile na ahadi zake zote zitamufunga.

13 Lakini kama mume wake atakaposikia habari zake, akizifunga na kuzivunja, basi, hata kama alitaka kutimiza kiapo au ahadi zake, hataombwa kuzitimiza. Mume wake atakuwa amezifunga na Yawe atamusamehe.

14 Mume wake anaweza kuhakikisha au kufunga kiapo au ahadi yoyote inayomufunga.

15 Lakini ikiwa mume wake hatasema neno lolote tangu siku atakaposikia habari za kiapo au ahadi ya muke wake, basi atakuwa ameihakikisha siku hiyo alipopata habari yake kwa sababu hakusema chochote.

16 Lakini akiifunga na kuivunja muda fulani nyuma ya kusikia habari yake, basi yeye atabeba lazima ya kosa la muke wake.

17 Haya ndiyo masharti ambayo Yawe alimwagiza Musa kati ya mume na muke wake, baba na binti yake, huyo binti akiwa bado kijana na anakaa katika nyumba ya baba yake.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan