Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hesabu 29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Sadaka ya sikukuu ya mwaka mupya
( Law 23.23-25 )

1 Siku ya kwanza ya mwezi wa saba, mutafanya mukutano mutakatifu. Musifanye kazi. Hiyo ni siku ya kupiga baragumu.

2 Mutatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote wakuwe wasiokuwa na kilema chochote.

3 Mutatoa vilevile sadaka yake ya vyakula ya unga safi uliochanganywa na mafuta: kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo dume,

4 na kilo moja kwa kila mwana-kondoo.

5 Tena mutatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho.

6 Mutatoa vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya mwezi mupya na sadaka yake ya vyakula, na sadaka ya kila siku ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji kama vile inavyoagizwa. Itakuwa harufu nzuri yenye kupendeza; ni sadaka kwa Yawe iliyoteketezwa kwa moto.


Matoleo ya siku ya kufanyiwa musamaha
( Law 23.26-32 )

7 Siku ya kumi ya mwezi wa saba mutafanya mukutano mutakatifu. Siku hiyo munapaswa kufunga kula na musifanye kazi.

8 Mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu ya kumupendeza Yawe: mwana-ngombe mumoja, kondoo dume mumoja, wana-kondoo saba wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.

9 Zaidi ya vitu hivi mutatoa sadaka ya unga safi uliochanganywa na mafuta kilo tatu pamoja na huyo ngombe dume, kilo mbili pamoja na yule kondoo dume,

10 na kilo moja kwa kila mwana-kondoo.

11 Mutatoa vilevile beberu mumoja kwa sadaka kwa ajili ya zambi zaidi ya sadaka ya kufanyiwa upatanisho, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji.


Sadaka ya sikukuu ya vibanda
( Law 23.33-43 ; Kumb 16.13-17 )

12 Siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mutafanya mukutano mutakatifu. Hamutafanya kazi siku hiyo. Mutafanya sikukuu kwa ajili ya Yawe kwa siku saba.

13 Mutatoa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, yenye harufu nzuri inayomupendeza Yawe: wana-ngombe dume kumi na watatu, kondoo dume wawili, wana-kondoo kumi na wane wa mwaka mumoja. Wote wasikuwe na kilema.

14 Sadaka itakayoandamana nazo itakuwa unga safi uliochanganywa na mafuta: kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo,

15 na kilo moja kwa kila mwana-kondoo.

16 Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

17 Siku ya pili mutatoa: wana-ngombe dume kumi na wawili, kondoo dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wane, wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema.

18 Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za vinywaji pamoja na wale wana-ngombe dume, kondoo na wana-kondoo, kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

19 Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya sadaka ya kuteketezwa ya kawaida pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

20 Siku ya tatu mutatoa: ngombe dume kumi na mumoja, kondoo wawili, wana-kondoo kumi na wane wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.

21 Mutawatolea pamoja na sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

22 Vilevile mutatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

23 Siku ya ine mutatoa: ngombe dume kumi, kondoo dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wane, wasiokuwa na kilema.

24 Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na hao ngombe dume na kondoo na wana-kondoo kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

25 Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

26 Siku ya tano, mutatoa ngombe dume tisa, kondoo wawili, wana-kondoo dume kumi na wane wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema.

27 Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na hao ngombe dume na kondoo na wana-kondoo kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

28 Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

29 Siku ya sita mutatoa ngombe dume wanane, kondoo dume wawili, wana-kondoo dume kumi na wane wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema.

30 Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na hao ngombe dume, kondoo dume na wana-kondoo kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

31 Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji.

32 Siku ya saba mutatoa ngombe dume saba, kondoo dume watatu, wana-kondoo dume kumi na wane wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema.

33 Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na hao ngombe dume, kondoo dume, na wana-kondoo, kulingana na hesabu yao, kama vile inavyoagizwa.

34 Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.

35 Siku ya nane mutakuwa na mukutano mutakatifu. Musifanye kazi siku hiyo.

36 Mutatoa sadaka ya kuteketezwa yenye harufu nzuri inayomupendeza Yawe: ngombe dume mumoja, kondoo dume mumoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema.

37 Mutatoa vilevile sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji pamoja na huyo ngombe dume, huyo kondoo dume, na wale wana-kondoo kulingana na hesabu yao kama vile inavyoagizwa.

38 Vilevile mutatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka ya kinywaji.

39 Haya ndiyo maagizo juu ya sadaka mutakazomutolea Yawe wakati wa sikukuu zenu zilizopangwa. Zaidi ya hizi zote, kuna vilevile sadaka za kuteketezwa, za vyakula na za kinywaji, za kutimiza kiapo na za mapenzi, na za amani.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan