Hesabu 28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Sadaka za kila siku ( Kut 29.38-46 ) 1 Yawe akamwambia Musa: 2 Uwaamuru Waisraeli maneno haya: Ninyi mutanitolea kwa wakati wake sadaka zinazotakiwa: vyakula vya kuteketezwa kwa moto, vyenye harufu nzuri ya kupendeza. 3 Uwaambie kwamba sadaka watakayonitolea ya kuteketezwa kwa moto, itakuwa hii: wana-kondoo wawili wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema chochote, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. 4 Mwana-kondoo mumoja atatolewa asubui na wa pili magaribi; 5 kila mumoja atatolewa pamoja na sadaka ya vyakula ya kilo moja ya unga uliochanganywa pamoja na litre moja ya mafuta bora yaliyopondwa. 6 Hii ni sadaka ya kutolewa kila siku inayoteketezwa kabisa kwa moto, ambayo ilitolewa kwa mara ya kwanza kwenye mulima Sinai kama sadaka ya ngano, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe. 7 Sadaka ya kinywaji itakayotolewa na kila mwana-kondoo ni litre moja ya divai. Utaimimina sadaka hii ya kinywaji kikali Pahali Patakatifu. 8 Wakati wa magaribi utamutoa yule mwana-kondoo mwingine kwa kuteketezwa kwa moto, pamoja na sadaka zile za ngano na za kinywaji. Itakuwa sadaka yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe. Sadaka za Sabato 9 Siku ya Sabato, mutatoa sadaka ya wana-kondoo dume wawili wa mwaka mumoja wasiokuwa na kilema, sadaka ya vyakula ya kilo mbili za unga laini uliochanganywa na mafuta, na sadaka yake ya kinywaji. 10 Sadaka hii ya kuteketezwa itatolewa kila siku ya Sabato zaidi ya ile sadaka ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji. Sadaka za kila mwezi 11 Kwa mwanzo wa kila mwezi, mutamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wasiokuwa na kilema. 12 Mutatoa sadaka ya vyakula ya unga laini kilo tatu, uliochanganywa na mafuta kwa kila ngombe dume mumoja; mutatoa kilo mbili za unga; kwa kila kondoo dume, 13 na kilo moja ya unga kwa kila mwana-kondoo. Sadaka hizi za kuteketezwa ni sadaka za chakula zenye harufu ya kumupendeza Yawe. 14 Kipimo cha sadaka ya kinywaji kinachohitajika ni litre mbili za divai kwa kila ngombe dume; litre moja na nusu kwa kila kondoo dume, na litre moja kwa kila mwana-kondoo. Hii ndiyo sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi katika mwaka muzima. 15 Tena mutamutolea Yawe sadaka kwa ajili ya zambi, beberu mumoja, zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kila siku na sadaka yake ya kinywaji. Sadaka za Pasaka ( Law 23.5-14 ) 16 Siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza ni Pasaka ya Yawe. 17 Siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni sikukuu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu. 18 Katika siku ya kwanza kutakuwa mukutano mutakatifu. Siku hiyo hamutafanya kazi. 19 Mutatoa sadaka ya kuteketezwa kama vile sadaka ya ngano kwa Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote wakuwe bila kilema. 20 Sadaka ya ngano itakayoandamana nazo itakuwa ya unga safi uliochanganywa na mafuta, kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo dume, 21 na kilo moja kwa kila mumoja wa wale wana-kondoo saba. 22 Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho. 23 Mutatolea vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kawaida inayotolewa kila siku asubui. 24 Vivyo hivyo, kwa muda wa siku saba, mutatoa kila siku sadaka ya ngano ya kuteketezwa. Itakuwa ni harufu nzuri ya kumupendeza Yawe. Hii mutaitoa zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kila siku na sadaka yake ya kinywaji. 25 Katika siku ya saba mutafanya mukutano mutakatifu; musifanye kazi. Sadaka ya sikukuu ya mavuno ( Law 23.15-22 ) 26 Katika siku ya kwanza ya sikukuu ya majuma wakati munapomutolea Yawe malimbuko ya ngano zenu, mutafanya mukutano mutakatifu; musifanye kazi. 27 Mutatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe: wana-ngombe dume wawili, kondoo dume mumoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mumoja, wote hao wakuwe bila kilema. 28 Sadaka ya ngano itakayoandamana nazo itakuwa ya unga safi uliochanganywa na mafuta kilo tatu kwa kila ngombe dume, kilo mbili kwa kila kondoo dume, 29 na kilo moja kwa kila mwana-kondoo. 30 Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho. 31 Mutatoa vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kawaida pamoja na sadaka yake ya kinywaji. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo