Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hesabu 26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Hesabu ya Pili

1 Kisha ule ugonjwa, Yawe akamwambia Musa na Eleazari mwana wa kuhani Haruni.

2 Muhesabu Waisraeli wote, kila mutu kufuatana na jamaa yake. Muwahesabu watu wote wenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi wanaofaa kwenda katika jeshi.

3 Musa na kuhani Eleazari wakazungumuza na watu kwenye inchi za mabonde za Moabu, ngambo ya muto Yordani, karibu na Yeriko, wakawaambia:

4 Muhesabu watu kuanzia na wenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa. Hesabu ya Waisraeli waliotoka Misri ni hii:

5 Kwanza ni kabila la Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Yakobo. Hanoki, Palu,

6 Hesironi na Karmi.

7 Hizo ndizo ukoo za kabila la Rubeni. Hesabu ya wanaume waliohesabiwa ni elfu makumi ine na tatu, mia saba na makumi tatu.

8 Wazao wa Palu walikuwa Eliabu,

9 na wana wake Nemueli, Datani na Abiramu. Hawa wawili: Datani na Abiramu, ndio waliokuwa wamechaguliwa, lakini wakamupinga Musa na Haruni, na kujiunga na wafuasi wa Kora wakati walipomwasi Yawe.

10 Wakati huo udongo ukafunguka ikawameza, wakakufa pamoja na Kora na wafuasi wake moto ulipoangamiza watu mia mbili makumi tano; wakakuwa onyo kwa watu.

11 Pamoja na hayo wana wa Kora hawakukufa.

12 Kabila la Simeoni. Nemueli, Yamini, Yakini,

13 Zera na Sauli.

14 Hizo ndizo ukoo za kabila la Simeoni, jumla yao wanaume elfu makumi mbili na mbili mia mbili.

15 Kabila la Gadi lilikuwa na jamaa za Sefoni, Hagi, Suni,

16 Ozini, Eri,

17 Arodi na Areli.

18 Hizo ndizo ukoo za kabila la Gadi, jumla wanaume elfu makumi ine mia tano.

19 Kabila la Yuda lilikuwa na Eri na Onani. Hawa walikufia katika inchi ya Kanana.

20 Kabila la Yuda lilikuwa na jamaa za Sela, Peresi, na Zera.

21 Kutoka kwa Peresi, jamaa ya Hesironi na Hamuli.

22 Hizo ndizo ukoo za Yuda, jumla wanaume elfu makumi saba na sita mia tano.

23 Kabila la Isakari lilikuwa na jamaa za Tola, Puva,

24 Yasubu na wa Simironi.

25 Hizo ndizo ukoo za Isakari, jumla wanaume elfu makumi sita na ine mia tatu.

26 Kabila la Zebuluni lilikuwa na jamaa za Seredi, wa Eloni na wa Yaleli.

27 Hizo ndizo ukoo za Zebuluni, jumla wanaume elfu makumi sita mia tano.

28 Kabila la Yosefu baba ya Manase na Efuraimu.

29 Kabila la Manase lilikuwa na jamaa ya: Makiri, Gileadi,

30 Yezeri, Heleki,

31 Asirieli, Sekemu,

32 Semida na Heferi.

33 Selofehadi mwana wa Heferi hakupata watoto wanaume lakini wanawake tu, nao ni Mala, Noa, Hogula, Milka na Tirsa.

34 Hizo ndizo ukoo za Manase, jumla wanaume elfu makumi tano na mbili mia saba.

35 Kabila la Efuraimu lilikuwa na jamaa za Sutela, Bekeri na Tahani.

36 Ukoo wa Erani ulikuwa na jamaa ya Sutela.

37 Hizo ndizo ukoo za Efuraimu, jumla wanaume elfu makumi tatu na mbili mia tano. Zote hizo zilitokana na Yosefu.

38 Kabila la Benjamina lilikuwa na jamaa za Bela, Asibeli, Ahiramu,

39 Sufamu na Hufamu.

40 Ukoo za Ardi na Namani, zilitokana na Bela.

41 Hizo ndizo ukoo za Benjamina, jumla wanaume elfu makumi ine na tano mia sita.

42 Kabila la Dani lilikuwa na jamaa ya Suhamu;

43 ukoo ulikuwa na wanaume elfu makumi sita na ine mia ine.

44 Kabila la Aseri lilikuwa na jamaa za Imuna, Isiwi na Beria.

45 Ukoo za Heberi na Malkieli zilitokana na Beria.

46 Aseri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.

47 Hizo ndizo ukoo za kabila la Aseri, jumla wanaume elfu makumi tano na tatu mia ine.

48 Kabila la Nafutali lilikuwa na jamaa za Yaseli, Guni,

49 Yeseri na Silemu.

50 Hizi ndizo ukoo za kabila la Nafutali, jumla wanaume elfu makumi ine na tano mia ine.

51 Hesabu ya wanaume Waisraeli waliohesabiwa ilikuwa elfu mia sita, na moja mia saba na makumi tatu.

52 Kisha Yawe akamwambia Musa:

53 Makabila haya yatagawanyiwa inchi ikuwe urizi wao, kulingana na hesabu ya majina yao.

54 Kabila kubwa litapewa sehemu yao kubwa na dogo litapewa sehemu yao ndogo. Kila kabila litapewa urizi wake kulingana na hesabu ya watu wake.

55 Hata hivyo ugawanyaji wa inchi utafanywa kwa kura. Kila kabila litarizi kulingana na majina ya ukoo wao.

56 Urizi wa kila kabila utagawanywa kwa kura, kila kabila litapata kulingana na ukubwa au udogo wake.

57 Hizi ndizo ukoo za Walawi zilizohesabiwa na jamaa zao Gersoni, Kohati na Merari,

58 pamoja na jamaa za Libini, Hebroni, Mali, Musi na Kora. Kohati alikuwa baba ya Amuramu.

59 Muke wa Amuramu aliitwa Yokebedi binti ya Lawi, aliyezaliwa Misri. Huyu alimuzalia Amuramu watoto wawili wanaume, Haruni na Musa, na binti mumoja, Miriamu.

60 Haruni alikuwa na watoto wanaume wane, Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.

61 Nadabu na Abihu walikufa walipomutolea Yawe sadaka ya moto usiofaa.

62 Hesabu ya Walawi wanaume wenye umri wa mwezi mumoja na zaidi ilikuwa elfu makumi mbili na tatu. Hawa hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu wao hawakupewa urizi wowote kati yao.

63 Hao ndio wanaume Waisraeli waliohesabiwa na Musa na kuhani Eleazari katika inchi za mabonde za Moabu, ngambo ya muto Yordani, karibu na Yeriko.

64 Kati yao hakukuwa hata mutu mumoja aliyebakia kati ya wale waliohesabiwa na Musa na kuhani Haruni ambao walifanya hesabu ya kwanza katika jangwa la Sinai.

65 Yawe alikuwa amesema kwamba wote watakufia katika jangwa, na kweli hakuna hata mumoja wao aliyebaki muzima, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan