Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hesabu 25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Waisraeli na Bali wa Peori

1 Waisraeli walipokuwa kule Sitimu, wanaume wakaanza kuzini na wanawake wa Moabu.

2 Wanawake hao waliwaalika Waisraeli washiriki matambiko waliyotambikia miungu yao, nao Waisraeli wakakula chakula na kuabudu miungu yao.

3 Ndivyo Waisraeli walivyojiunga na mungu Bali wa Peori, nayo hasira ya Yawe ikawaka juu yao.

4 Basi, Yawe akamwambia Musa: Utwae viongozi wote wa Israeli, uwatundike mbele yangu jua kati, kusudi kasirani yangu juu yenu ipite.

5 Musa akawaambia waamuzi wa Israeli: Kila mumoja wenu amwue mutu yeyote kati yenu ambaye amejiunga na mungu Bali wa Peori.

6 Wakati huohuo mutu mumoja akamuleta mwanamuke mumoja Mumidiani katika nyumba yake, Musa na Waisraeli wote pamoja wakiwa wanaomboleza kwenye mulango wa hema la mukutano.

7 Basi, Finehasi mwana wa Eleazari mujukuu wa kuhani Haruni alipoona hayo, akasimama, akatoka, akatwaa mukuki

8 na kumufuatilia yule Mwisraeli mpaka ndani ya hema, akawachoma mukuki wote wawili ndani ya tumbo. Ugonjwa mukali uliokuwa umewaangamiza Waisraeli ukakomeshwa.

9 Waliokufa kutokana na ugonjwa ule mukali walikuwa watu elfu makumi mbili na ine.

10 Yawe akamwambia Musa:

11 Finehasi mwana wa Eleazari, mujukuu wa kuhani Haruni, ameizuia hasira yangu juu ya Waisraeli; kati yenu ni yeye tu aliyeona wivu kama ule ninaokuwa nao mimi. Ndiyo maana sikuwaangamiza Waisraeli wote kwa hasira yangu.

12 Kwa hiyo umwambie kwamba ninafanya naye agano la amani.

13 Ninaagana naye kwamba yeye na wazao wake watakuwa makuhani milele kwa sababu aliona wivu kwa ajili yangu mimi Mungu wake, akawafanyia Waisraeli upatanisho.

14 Huyo Mwisraeli aliyeuawa pamoja na mwanamuke wa Kimidiani aliitwa Zimuri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa moja katika kabila la Simeoni.

15 Na huyo mwanamuke Mumidiani aliyeuawa aliitwa Kozibi binti ya Suri, aliyekuwa kiongozi wa ukoo fulani huko Midiani.

16 Yawe akamwambia Musa:

17 Uwachokoze Wamidiani na kuwaangamiza,

18 kwa sababu waliwachokoza ninyi kwa werevu wao, ambao kwa njia yake wamewadanganya katika jambo la Peori, na kwa sababu ya Kozibi, binti yao, aliyeuawa wakati ugonjwa mukali ulipotokea kule Peori.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan