Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Hesabu 13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Wapelelezi
( Kumb 1.19-33 )

1 Yawe akamwambia Musa:

2 Tuma watu waende wapeleleze inchi ya Kanana ambayo ninawapa watu wa Israeli. Utatuma mutu mumoja kutoka katika kila kabila, na mutu huyo anapaswa kuwa kiongozi katika kabila lake.

3 Basi, kwa agizo la Yawe, Musa akatuma watu kutoka jangwa la Parani. Watu wote waliotumwa walikuwa viongozi wa makabila mbalimbali ya watu wa Israeli.

4-15 Haya ndiyo majina ya watu hao kulingana na makabila yao: Kabila la Rubeni: Samua mwana wa Zakuri. Kabila la Simeoni: Safati mwana wa Hori. Kabila la Yuda: Kalebu mwana wa Yefune. Kabila la Isakari: Igali mwana wa Yosefu. Kabila la Efuraimu: Hosea mwana wa Nuni. Kabila la Benjamina: Palti mwana wa Rafu. Kabila la Zebuluni: Gadieli mwana wa Sodi. Kabila la Yosefu (ni kusema kabila la Manase): Gadi mwana wa Susi. Kabila la Dani: Amieli mwana wa Gemali. Kabila la Aseri: Seturi mwana wa Mikaeli. Kabila la Nafutali: Nabi mwana wa Wofusi. Kabila la Gadi: Geueli mwana wa Maki.

16 Haya ndiyo majina ya watu ambao Musa aliwatuma kwenda kupeleleza inchi ya Kanana. Musa akamupa Hosea mwana wa Nuni jina jipya, akamwita Yoshua.

17 Alipowatuma kwenda kupeleleza inchi ya Kanana, Musa akawaambia: Muende kule ngambo Negebu, mpaka kwenye inchi ya milima,

18 mupeleleze jinsi inchi inavyokuwa. Muchunguze vilevile kama watu wanaoishi mule ni wenye nguvu au wazaifu, wengi au wachache.

19 Mupeleleze kama inchi hiyo ni nzuri au mbaya, na kama miji wanamoishi ni kambi au ni nyumba zilizozungukwa na kuta.

20 Muchunguze vilevile kama inchi yenyewe ni tajiri au masikini, ina miti au haina. Mukuwe na mioyo ya ushujaa na munaporudi mulete matunda ya inchi hiyo. Ilikuwa ni wakati zabibu zinapoanza kuivya.

21 Basi, watu hao wakaenda na kupeleleza inchi toka jangwa la Sini mpaka Rehobu, karibu na njia ya kuingilia Hamati.

22 Wakakwenda mpaka Negebu wakapita mpaka muji wa Hebroni. Humo wakawakuta Waahimani, Wasesai na Watalmai, wazao wa Anaki. (Muji wa Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba mbele ya muji wa Soani unaokuwa katika inchi ya Misri).

23 Walipofika katika Bonde la Eskoli, watu hao wakakata shada la muzabibu lililokuwa na matunda mengi nalo lilibebwa na watu wawili juu ya muti. Wakatwaa vilevile makomamanga na tini.

24 Pahali pale pakaitwa Bonde la Eskoli, ni kusema “Bonde la Shada” kwa sababu ya shada ambalo watu hao wa Israeli walikata kutoka pahali pale.

25 Kisha kupeleleza inchi kwa muda wa siku makumi ine, watu hao wakarudi.

26 Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.

27 Wakamwambia Musa: Tuliifikia inchi uliyotutuma tuipeleleze; hiyo ni inchi inayotiririka maziwa na asali, na hili ni tunda lake.

28 Lakini wenyeji wake ni wenye nguvu sana, na miji yao ni imara na mikubwa sana. Zaidi ya hayo, huko tuliona wazao wa Anaki.

29 Waamaleki wanakaa katika eneo la Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanakaa katika eneo la milima, na Wakanana wanakaa karibu na bahari ya Mediteranea na karibu na kingo za muto Yordani.

30 Lakini Kalebu akanyamazisha watu mbele ya Musa, akasema: Tuende mara moja tuitwae inchi hiyo. Kwa sababu tuko na uwezo sana wa kushinda.

31 Lakini watu walioandamana naye kupeleleza inchi wakasema: Hatutaweza kupigana na watu hao; wao wana nguvu kuliko sisi.

32 Kwa hiyo wakaeneza mambo ya uongo kati ya watu wa Israeli juu ya inchi waliyoipeleleza, wakisema: Inchi hiyo inawaua watu wake. Vilevile watu wote tuliowaona huko ni wakubwa sana.

33 Tuliona majitu huko, wazao wa Anaki. Sisi tulijiona kuwa kama mapanzi mbele yao, na ndivyo walivyotuona sisi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan