Hesabu 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Miriamu anaazibiwa 1 Kisha Miriamu na Haruni wakaanza kumusema Musa vibaya kwa sababu ya mwanamuke Mukushi aliyekuwa amemwoa. 2 Wakasema: Basi, Yawe amezungumuza kwa kumwagiza Musa peke yake? Si amezungumuza nasi vilevile? Yawe akasikia maneno hayo. 3 (Musa alikuwa mutu munyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa katika dunia.) 4 Halafu kwa rafla, Yawe akawaambia Musa, Haruni na Miriamu: Mukuje katika hema la mukutano, ninyi watatu. Basi, wote watatu wakaenda kwenye hema la mukutano. 5 Hapo Yawe akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye mulango wa hema, akawaita Haruni na Miriamu. Wote wawili wakasogea mbele. 6 Kisha Yawe akawaambia: Musikilize maneno yangu, kama kuna nabii kati yenu, mimi Yawe ninajifahamisha kwake katika maono na kuongea naye katika ndoto. 7 Lakini juu ya mutumishi wangu Musa, hali ni tofauti kabisa. Yeye ana madaraka ya kuwatunza watu wangu wote. 8 Mimi ninaongea naye kinywa kwa kinywa, waziwazi na si kwa kutumia mafumbo. Yeye ameliona umbo langu mimi Yawe. Kwa nini, basi, hamukuogopa kusema vibaya juu ya mutumishi wangu Musa? 9 Hapo Yawe akawaka hasira juu yao, akaondoka, akaenda zake. 10 Wingu lilipoondoka juu ya hema la mukutano, Miriamu akaonekana yuko na ukoma, mweupe kama teluji. Haruni alipogeuka na kumwangalia Miriamu, akashangaa kuona kwamba ameshikwa na ukoma. 11 Hapo, Haruni akamwambia Musa: Ewe bwana wangu, tumetenda mambo ya kipumbafu na kufanya zambi. Lakini usituazibu! 12 Usimufanye Miriamu akuwe kama mutu aliyezaliwa mufu, ambaye karibu nusu ya mwili wake imeozeshwa. 13 Musa akamulilia Yawe akisema: Ninakusihi, ee Mungu, umuponye. 14 Lakini Yawe akamwambia Musa: Kama baba yake angemutemea mate kwenye uso, basi, hangepata haya kwa siku saba? Basi, umutoe inje ya kambi akae kule muda wa siku saba, kisha unaweza kumuruhusu arudi katika kambi. 15 Kwa hiyo, Miriamu akafukuzwa inje ya kambi kwa muda wa siku saba. Watu hawakuanza tena safari mpaka Miriamu aliporudishwa tena katika kambi. 16 Nyuma ya hayo, watu wakafanya safari kutoka Haseroti, wakapiga kambi katika jangwa la Parani. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo