Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Filemono 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Salamu

1 Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo, na kwa ndugu yetu Timoteo. Tunakuandikia wewe Filemono, mupendwa wetu na mwenzetu wa kazi,

2 na kanisa linalokusanyika katika nyumba yako, na dada yetu Apia na Arkipo mupiganaji mwenzetu wa vita.

3 Tunawatakia neema na amani toka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.


Upendo na imani ya Filemono

4 Ninamushukuru Mungu wangu siku zote nikikukumbuka wewe Filemono katika maombi yangu.

5 Kwa maana ninasikia namna unavyomwamini Bwana Yesu na namna unavyowapenda watu wote wa Mungu.

6 Ninamwomba Mungu kwamba ushirika wa imani yako uzae matunda, na kwa njia hiyo upate kujua mema yote tunayokuwa nayo katika kuungana kwetu na Kristo.

7 Ndugu, upendo wako umenifurahisha sana na kunifariji, kwa maana umetuliza mioyo ya watu wa Mungu.


Paulo anamwombea Onesimo

8 Kwa sababu hii, ingawa ninakuwa na mamlaka niliyopewa na Kristo kukuagiza neno unalopaswa kufanya,

9 lakini kwa ajili ya upendo, ninapendelea kukusihi, mimi Paulo ninayekuwa muzee, na zaidi sasa ninakuwa mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo.

10 Ninakusihi kwa ajili ya mutoto wangu Onesimo, niliyemuzaa katika imani nikiwa katika kifungo.

11 Zamani yeye hakukufalia kitu, lakini sasa atakufalia wewe na mimi vilevile.


Maagizo na salamu za mwisho

12 Sasa ninamurudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.

13 Ningalipenda Onesimo abakie pamoja nami kwa kunisaidia pahali pako wakati ninapokuwa mufungwa kwa sababu ya Habari Njema.

14 Lakini sikutaka kufanya kitu chochote pasipo shauri lako. Wala sikutaka kukulazimisha unitendee mema; lakini ningetaka uyatende kwa mapenzi yako mwenyewe.

15 Labda hii ndiyo sababu Onesimo aliachana nawe kwa muda, kusudi upate tena kuwa naye siku zote.

16 Kwa sababu sasa yeye si kama vile mutumwa tu, lakini amekuwa bora zaidi kuliko mutumwa: yeye ni ndugu mupendwa. Mimi ninamupenda sana, nawe utamupenda zaidi sana, kwanza kama vile mutumwa, tena kama vile ndugu katika Bwana.

17 Basi kama unaendelea kunihesabu kuwa mwenzako, umupokee kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.

18 Kama alikukosea au kama yuko na deni yako ya kitu chochote, unidai mimi.

19 Mimi Paulo ninaandika kwa mukono wangu mwenyewe maneno haya: nitakulipa. (Sitaki kusema kwamba maisha yako ni deni unalokuwa nalo kwangu.)

20 Ndiyo, ndugu yangu, ninakusihi unisaidie kwa njia hii kwa ajili ya Bwana, unitulize moyo kama vile ndugu katika Kristo.

21 Ninapokuandikia, nina uhakika kwamba utanisikia na hata utafanya zaidi kuliko vile nilivyosema.

22 Lakini pamoja na maneno haya, unitayarishie vilevile pahali pa kukaa, maana ninatumaini kwamba Mungu atajibu maombi yenu, na kunijalia nipate kurudishwa tena kwenu.

23 Epafra, mufungwa mwenzangu, kwa ajili ya Yesu Kristo, anakusalimia.

24 Vilevile Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanya kazi wenzangu, wanakusalimia.

25 Ninawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan