Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Ezra 9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Waisraeli wanaoa wanawake wa kigeni Kurudi Yerusalema

1 Nyuma ya mambo haya yote kutendeka, viongozi wakanifikia na kunipa habari hii: “Watu wa Israeli, makuhani na Walawi hawakujitenga na wakaaji wa inchi ambao wanatenda machukizo: Waamoni, Wamoabu na Wamisri, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wayebusi na Waamori.

2 Wayuda wanaoa wanawake wa kigeni na kuwaoea wana wao vilevile. Hivyo, taifa takatifu la Mungu limechanganyika na watu wa mataifa mengine. Vilevile wasimamizi na wakubwa ndio wa kwanza kutenda maovu hayo.”

3 Nilipoyasikia maelezo hayo, nikapasua nguo zangu na koti langu, nikaongoa nywele zangu na ndevu zangu kwa huzuni kubwa na kuikaa chini na kufazaika.

4 Halafu watu wote walioshikwa na hofu kwa sababu ya maneno Mungu wa Israeli aliyosema juu ya makosa ya wale waliorudi kutoka katika uhamisho wakaanza kukusanyika karibu nami nikiwa mwenye kufazaika mpaka magaribi, wakati wa kutoa sadaka.

5 Magaribi, wakati wa kutoa sadaka ulipofika, nikasimama pahali pale nilipokuwa nimeikaa kwa huzuni nazo nguo zangu zimepasuka pamoja na koti, nikapiga magoti na kunyoosha mikono yangu kwa Yawe, Mungu wangu, na kuomba,

6 nikisema: “Ee Mungu wangu, ninaona haya kubwa sana kukiinua kichwa changu mbele yako. Zambi zetu zimelundikana kupita hata vichwa vyetu; makosa yetu yanafika hata mbinguni.

7 Tangu nyakati za babu zetu mpaka sasa, sisi watu wako tumekukosea sana. Na kwa sababu ya zambi zetu, sisi, wafalme wetu na makuhani wetu tulitiwa katika mikono ya wafalme wa inchi za kigeni, tukauawa, tukapelekwa kuwa wafungwa na kunyanganywa mali zetu. Na hata hivi leo, tumetiwa haya kupita kiasi.

8 Lakini sasa, ee Yawe, Mungu wetu, kwa muda mufupi umetuonyesha huruma yako na kuwawezesha wamoja kati yetu kuponyoka kutoka katika utumwa na kuishi kwa usalama pahali pako patakatifu. Pahali pa utumwa, umetupa furaha na maisha mapya.

9 Haukutuacha tuishi katika utumwa ingawa tulikuwa watumwa. Uliwafanya wafalme wa Persia wakuwe wema kwetu na kuturuhusu tuishi na kuijenga nyumba yako iliyokuwa imebomoka, na ukatufanya tukae salama hapa Yuda na Yerusalema.

10 “Lakini sasa, ee Mungu wetu, tuseme nini nyuma ya hayo yote? Maana, tumeziasi amri zako

11 ulizotupa kwa njia ya watumishi wako manabii ukisema: ‘Inchi munayoiendea na ambayo itakuwa mali yenu ni inchi chafu, yenye uchafu wa wakaaji toka inchi mbalimbali, kwa machukizo yao, wameijaza uchafu tele, kila nafasi.

12 Kwa hiyo, musiwaoeshe na wabinti zenu kwa watu hao, wala musiwaruhusu wana wenu kuwaoa wabinti zao. Pia, musishugulikie usalama au mafanikio yao, kusudi ninyi wenyewe mupate kuwa na nguvu, na mufaidie mema ya inchi hiyo na kuwaachia watoto wenu kama vile urizi milele.’

13 Hata nyuma ya yote yaliyotupata kwa sababu ya maovu yetu na makosa yetu mengi, tunajua kwamba azabu uliyotupa, ee Mungu wetu, ni ndogo ikilinganishwa na makosa yetu, na umewaacha wazima wamoja kati yetu.

14 Tutavunja amri zako tena na kuoana na watu hawa wanaotenda maovu haya? Hautatukasirikia na kutuangamiza kabisa, na kusibaki hata mumoja wetu muzima wala yeyote wa kutoroka?

15 Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan