Ezra 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Watu waliorudi kutoka katika uhamisho (Neh 7.4-73) 1 Hawa ndio watu wa majimbo waliotoka katika utumwa ambao Nebukadneza mufalme wa Babeli aliwapeleka wafungwa Babeli, wakarudi katika Yerusalema katika inchi ya Yuda. Kila mutu alirudi katika muji wake. 2 Viongozi wao walikuwa Zerubabeli, Yesua, Nehemia, Seraya, Relaya, Mordekayi, Bilsani, Misipari, Bigwayi, Rehumu na Bana. Hii ndiyo hesabu ya watu wote wa ukoo za Waisraeli waliorudi kutoka katika uhamisho: 3 wa ukoo wa Parosi: elfu mbili mia moja makumi saba na wawili; 4 wa ukoo wa Sefatia: mia tatu makumi saba na wawili; 5 wa ukoo wa Ara: mia saba makumi saba na watano; 6 wa ukoo wa Pahati-Moabu, maana yake wazao wa Yesua na Yoabu: elfu mbili mia nane kumi na wawili; 7 wa ukoo wa Elamu: elfu moja mia mbili makumi tano na wane; 8 wa ukoo wa Zatu: mia tisa makumi ine na watano; 9 wa ukoo wa Zakayi: mia saba na makumi sita; 10 wa ukoo wa Bani: mia sita makumi ine na wawili; 11 wa ukoo wa Bebayi: mia sita makumi mbili na watatu; 12 wa ukoo wa Azgadi: elfu moja mia mbili makumi mbili na wawili; 13 wa ukoo wa Adonikamu: mia sita makumi sita na sita; 14 wa ukoo wa Bigwayi: elfu mbili na makumi tano na sita; 15 wa ukoo wa Adini: mia ine makumi tano na wane, 16 wa ukoo wa Ateri, ndiye Hezekia: makumi kenda na wanane; 17 wa ukoo wa Besayi: mia tatu makumi mbili na watatu; 18 wa ukoo wa Yora: mia moja kumi na wawili; 19 wa ukoo wa Hasumu: mia mbili makumi mbili na watatu; 20 wa ukoo wa Gibari: makumi kenda na watano. 21 Watu wa muji wa Betelehemu: mia moja makumi mbili na watatu; 22 wa muji wa Netofa: makumi tano na sita; 23 wa muji wa Anatoti: mia moja makumi mbili na wanane; 24 wa muji wa Azimaweti: makumi ine na wawili; 25 wa muji wa Kiriati-Yearimu, wa Kefira na wa Beroti: mia saba makumi ine na watatu; 26 wa muji wa Rama na wa Geba: mia sita makumi mbili na mumoja; 27 wa muji wa Mikimasi: mia moja makumi mbili na wawili; 28 wa muji wa Beteli na Ai: mia mbili makumi mbili na watatu; 29 wa muji wa Nebo: makumi tano na wawili; 30 wa muji wa Magibisi: mia moja makumi tano na sita; 31 wa muji wa Elamu wa pili: elfu moja mia mbili makumi tano na wane; 32 wa muji wa Harimu: mia tatu na makumi mbili; 33 wa muji wa Lodi, Hadidi na wa Ono: mia saba makumi mbili na watano; 34 wa muji wa Yeriko: mia tatu makumi ine na watano; 35 wa muji wa Sena: elfu tatu mia sita na makumi tatu. 36 Hii ndiyo jumla ya makuhani waliorudi kutoka katika uhamisho: wa ukoo wa Yedaya waliokuwa wazao wa Yesua: mia tisa makumi saba na watatu; 37 wa ukoo wa Imeri: elfu moja na makumi tano na wawili; 38 wa ukoo wa Pashuri: elfu moja mia mbili makumi ine na saba; 39 wa ukoo wa Harimu: elfu moja na kumi na saba. 40 Walawi wa ukoo wa Yesua na wa Kadimieli, wazao wa Hodavia waliorudi kutoka katika uhamisho walikuwa makumi saba na wane. 41 Waimbaji (wazao wa Asafu), walikuwa mia moja makumi mbili na wanane. 42 Walinzi wa mulango (wazao wa Salumu, wa Ateri, wa Talmoni, wa Akubu, wa Hatita na wa Sobayi), walikuwa mia moja makumi tatu na tisa. 43-54 Hizi ni ukoo za watumishi wa hekalu waliorudi kutoka katika uhamisho: Siha, Hasufa, Tabaoti, Kerosi, Siaha, Padoni, Lebana, Hagaba, Akubu, Hagabu, Semaya, Hanani, Gideli, Gahari, Raya, Resini, Nekoda, Gazamu, Uza, Pasea, Besayi, Asina, Munimu, Nefisimu, Bakuki, Hakufa, Harihuri, Basiluti, Mehida, Harsa, Barkosi, Sisera, Tema, Nezia, Hatifa. 55-57 Kati ya wazao wa watumishi wa Solomono, waliorudi kutoka katika uhamisho, kulikuwa wazao wa watu hawa: Sotayi, Hasofereti, Peruda, Yala, Darkoni, Gideli, Sefatia, Hatili, Pokereti-Hazebaimu, Ami. 58 Watumishi wote wa hekalu na wazao wa watumishi wa Solomono waliorudi kutoka katika uhamisho walikuwa watu mia tatu makumi kenda na wawili. 59 Watu walirudi kutoka miji hii: Teli-Mela, Teli-Harsa, Kerubu, Adani na Imeri. Lakini hawakuweza kuhakikisha kwamba walikuwa wazao wa Waisraeli. 60 Wao walikuwa watu wa ukoo wa Delaya wa Tobia na wa Nekoda, kwa jumla watu mia sita makumi tano na wawili. 61 Watu wa ukoo hizi za makuhani vilevile walirudi: ukoo wa Habaya, wa Hakosi na wa Barzilayi. Huyo Barzilayi alikuwa ameoa binti ya Barzilayi wa Gileadi, naye vilevile akaitwa Barzilayi. 62 Hao walitafuta ukoo wao katika kitabu cha ukoo, lakini hawakuonekana humo. Kwa hiyo hawakuruhusiwa kushika ukuhani maana walihesabiwa kuwa wachafu. 63 Mutawala akawaambia kwamba hawaruhusiwi kushiriki chakula kitakatifu sana, mpaka kukuwe kuhani atakayeweza kutoa shauri kwa njia Urimu na Tumimu. 64-67 Hii ni jumla ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho, pamoja na watumishi na nyama wao: Waisraeli: elfu makumi ine na mbili, mia tatu na makumi sita. Watumishi wanaume na wanawake: elfu saba mia tatu makumi tatu na saba. Waimbaji wanaume na wanawake: mia mbili. Farasi: mia saba makumi tatu na sita. Nyumbu: mia mbili makumi ine na watano. Ngamia: mia ine makumi tatu na watano. Punda: elfu sita mia saba na makumi mbili. 68 Watu hao waliotoka katika uhamisho, walipofika kwenye nyumba ya Yawe katika Yerusalema, viongozi wamoja wa ukoo hizo walitoa matoleo ya mapenzi kwa kusaidia ujenzi wa nyumba ya Mungu katika Yerusalema. 69 Walitoa kila mutu kadiri ya uwezo wake kwa ajili ya kazi hii. Jumla ya matoleo hayo ilikuwa kilo mia tano za zahabu, kilo elfu mbili na mia nane za feza na nguo mia moja kwa ajili ya makuhani. 70 Basi, makuhani, Walawi na watu wengine wamoja wakaanza kuishi katika Yerusalema na katika vijiji vyake. Nao waimbaji, walinzi wa hekalu na watumishi wa hekalu wakaanza kuishi katika miji yao; Waisraeli wote wakaishi katika miji yao. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo