Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Ezekieli 9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuazibiwa kwa Yerusalema

1 Kisha nikamusikia Yawe akisema kwa sauti kubwa: Mujongee karibu ninyi mutakaouazibu muji huu. Mukuje na silaha zenu za kuangamiza.

2 Watu sita wakakuja kutoka upande wa mulango wa juu unaoelekea upande wa kaskazini, kila mumoja na silaha yake ya kuangamiza katika mukono wake. Pamoja nao, kulikuwa mutu mumoja ambaye alikuwa amevaa nguo ya kitani, naye ana chupa la wino. Wakaingia ndani ya hekalu, wakasimama pembeni ya mazabahu ya shaba.

3 Kisha utukufu wa Mungu wa Israeli uliondoka pale juu ya makerubi na kupanda juu mpaka kwenye kizingiti cha nyumba ya Yawe. Yawe akamwita mutu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani, mwenye chupa la wino,

4 akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.

5 Kisha akawaambia wale wengine mimi nikiwa ninasikia: Mupite katika muji, muue watu; musimwachilie mutu yeyote wala kuwa na huruma.

6 Muwaue wazee palepale, vijana wanaume na wabinti, watoto na wanawake; lakini kila mumoja mwenye kuwa na kitambulisho, musimuguse. Muanzie katika hekalu langu. Basi, wakaanza na wazee waliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe.

7 Akawaambia: Muchafue nyumba ya Yawe kwa kuvijaza viwanja vyake maiti, kisha musonge mbele. Basi, wakaenda, wakawaua watu katika muji.

8 Wakati walipokuwa wakiwaua, mimi niliachwa peke yangu, nikaanguka uso mpaka chini, nikalia: Ee Bwana wangu Yawe, utaangamiza watu wote wa Israeli waliobaki, ukitimiza kasirani yako juu ya Yerusalema?

9 Naye akaniambia: Uovu wa Waisraeli na watu wa Yuda ni mukubwa sana. Inchi imejaa umwagaji wa damu na katika muji hakuna haki, kwa maana wanasema: Yawe ameiachilia inchi; Yawe haoni.

10 Kwa upande wangu, sitawaachilia wala kuwahurumia; nitawatendea kufuatana na matendo yao.

11 Kisha mutu yule aliyevaa nguo ya kitani, mwenye chupa la wino, akarudi na kutoa habari hii: Nimefanya kama ulivyoniamuru.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan