Ezekieli 4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Muji Yerusalema utashambuliwa 1 Yawe akaniambia tena: Wewe mwanadamu, twaa tofali, uliweke mbele yako na uchape juu yake muji, kama wa Yerusalema. 2 Onyesha kwamba muji ule umeshambuliwa. Utaujengea nafasi za kupandia juu ya kuta zake. Kandokando yake uweke makambi ya waaskari, na gongo ya kubomoa kuta. 3 Nawe utwae bamba la chuma. Ulisimamishe likuwe kama ukuta wa chuma kati yako na muji. Kisha utaelekezea muji huo uso wako nao utashambuliwa na utaushambulia. Hiki kitakuwa kitambulisho kwa taifa la Waisraeli. 4 Kisha, uende ulalie mbavu kwa upande wako wa kushoto. Muda wote utakapokaa katika hali hiyo utabeba uovu wa Waisraeli kama muzigo muzito. 5 Nimekupangia muda wa siku mia tatu na makumi kenda. Muda huu ni sawa na miaka ya azabu yao: siku moja ni sawa na mwaka mumoja. Utabeba azabu ya Waisraeli kwa muda huu. 6 Utakapotimiza siku hizo, utalalia kwa upande wa kuume, na hapo utabeba azabu ya watu wa ufalme wa Yuda kwa muda wa siku makumi ine; nimekupangia siku moja kuwa sawa na mwaka mumoja. 7 Kisha, utauelekea Yerusalema ulioshambuliwa kwa vita na kuunyooshea mukono mutupu na kutabiri juu yake. 8 Nitakufunga kamba kusudi usiweze kugeuka toka upande mumoja mpaka upande mwingine, mpaka wakati kushambuliwa kwa Yerusalema kutakapomalizika. 9 Wewe utwae ngano, shayiri, mahalagi, manjegere, mutama na ulezi, uvitie vyote katika chombo kimoja, ujitengenezee mukate. Mukate huo ndio utakaokuwa chakula chako wakati unapolala kwa upande mumoja, siku zote mia tatu na makumi kenda. 10 Chakula utakachokula kitapimwa, nacho kitakuwa grama mia mbili makumi tatu kwa siku; nawe utakula mara moja tu kwa siku. 11 Maji nayo utayakunywa kwa kipimo: vikombe viwili, mara moja kwa siku. 12 Utatwaa mavi ya mutu, uwashe nayo moto, upike mukate juu yake na kuukula mbele ya watu. 13 Yawe aliniambia: Vile ndivyo Waisraeli watakavyokula mukate wao muchafu wakiwa kati ya mataifa ninakowapeleka. 14 Halafu nikamwambia hivi: Ee, Bwana wangu Yawe, sijajichafua hata kidogo kwa kula nyamafu wala nyama aliyeuawa na nyama wa pori, wala sijapata kuonja nyama anayehesabiwa kuwa muchafu tangu ujana wangu. 15 Kisha akaniambia: Basi, ninakuruhusu utumie mavi ya ngombe pahali pa mavi ya mutu kwa kupika mukate wako. 16 Tena akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, mimi nitaharibu akiba ya chakula katika Yerusalema; wakaaji wake watakula chakula watakachopimiwa kwa hofu. Watakunywa maji watakayopimiwa kwa kufazaika. 17 Nitafanya hivyo kusudi wakose chakula na maji, na kila mumoja atamwangalia mwenzake kwa kufazaika; nao watakuwa zaifu kwa ajili ya azabu yao. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo